Mahaba ya Snura awapo Sita kwa Sita yatishia kuvunja kitanda



Staa  wa  kike  anayetikisa  kwenye  tasnia  ya  filamu  na  muziki, Snura  Mushi  a.k.a  Majanga  anadaiwa  kuwa  ni  mmoja  wa  mastaa  wa  kike  wenye  ujuzi  mkubwa  kimahaba  kiasi  cha  kuwapagawisha mno  wanaume  anaokuwa  nao  katika  mahusiano.....

Chanzo  chetu  cha habari  ambacho  kiko  karibu  na  staa  huyo  kilieleza  kuwa  Snura  huwa  na  tabia  ya  kupandisha  mzuka  wa  jukwaani  awapo  kwenye  sita  kwa  sita  na  wakati  mwingine  huweza  hata  kuvunja  kitanda  endapo  akiamua  kufanya  hivyo.....

"Unajua  Snura  anaasili  ya  kizaramo, Amefundwa  kila  aina  ya  mafunzo  ya  kuwa  na  mwanaume.Mimi  ni  rafiki  yangu  kwa  kipindi  kirefu, yaani  tokea  niwe  karibu  naye  wanaume  aliowahi  kuwa  nao  wamemsifu  kuwa  anaweza  mambo  tena  si  kitoto", Kilieleza  chanzo  hicho
Inadaiwa  kwamba  asilimia  kubwa  ya  mastaa  wa  kike  huwa  hawapendi  kujishughulisha  wawapo  faragha  kutokana  na  ustaa  wao,lakini  taarifa  za  Snura  zimekuwa  tofauti....

Mwandishi  wetu  alimtafuta  Snura  ambaye  baada  ya  kumuuliza  aliangua  kicheko:

"Sasa  utamu  wa  ngoma  si  ni  lazima  uicheze? Huwezi  kujua  hivi  hivi.Hayo  mambo  ni  mazito  sana  naona  kwangu  ni  ngumu  kuyazungumzia  kwa  sababu  najiandaa  kuolewa. Ila  kwa  mwanamke  hasa  wa  taipu  yangu  ni  lazima  ujue  kumpetipeti  mume.

"Hilo  halinipi  shida  sana  sababu  nimekamilika  kila  idara.Mbele  ya  watu  kibao  shughuli  inakuwa  pevu  jukwaani  sembuse  chumbani  wawili  tu?"  Alisema  staa  huyo  anayefunika  Tanzania  na  ngoma  yake  ya  Nimevurugwa