Trafiki Anusurika kufa baada ya Kuvaana Uso kwa Uso na Gari Dogo eneo la Bamaga Mikocheni jijini Dar es salaam


Askari mmoja wa kikosi cha usalama barabara ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja amenusurika kufa baada ya kupata ajali akiwa anaendesha pikipiki ya polisi ambayo ilikosa mwelekeo na kugongana uso kwa uso na gari dogo lenye namba za usajili T 681 CUX eneo la Bamaga Mikocheni jijini Dar es salaam ambapo gari hilo lilikuwa likiandeshwa na mwanamke mmoja huku mashuhuda wa ajali hiyo kila mmoja akiwa na mtazamo tofauti juu ya ajali hiyo.

Irene Uwoya amtaka Ndikumana Yanga, mwenyewe aogopa kulogwa.....Asema Uwoya bado ni Mke wake na wanapendana sana


BINTI aliyejaliwa uzuri wa sura anayeng’ara kwenye filamu za Kibongo, anamshawishi mumewe Hamad Ndikumana aje kucheza Yanga ya chini ya kocha, Marcio Maximo.
 
Ndikumana ambaye kwa sasa anaichezea Vital’o ya Bujumbura, Burundi ameweka wazi kwamba binti huyo, Irene Uwoya ambaye ni mkewe ni shabiki wa Jangwani na amekua akimshawishi kila mara kwamba atue Jangwani ili awe naye karibu zaidi kwani hana mpango wa kuondoka Dar es Salaam kwenye kazi zake za filamu.
 
Mchezaji huyo amekiri kushawishiwa mara nyingi lakini alisema hawezi kujipeleka Yanga mpaka timu hiyo itakapomfuata, kama hiyo haitoshi aliongeza kwamba anaogopa kuishi Dar es Salaam kutokana na mambo ya ushirikina yaliyomtokea alipoanza maisha na mkewe ambaye ameshangaa watu wanaozusha kwamba wameachana.
 
“Ananitaka nije kucheza Tanzania alikuwa ananiambia nije Yanga, unajua anaipenda sana Yanga lakini nikamwambia mimi ni mchezaji ninayejiamini siwezi kuja kuomba Yanga wanisajili acha waje wao tuzungumze, yuko tayari kufanya hata ushawishi kwa wadau,” anasisitiza Ndikumana ambaye awali alikuwa akiichezea APOP Kinyras Peyias ya Cyprus.
 
Ndikumana alisema kilichomtoa Cyprus na kuja Burundi pamoja na uhusiano wake na Uwoya.
 
“Kweli nilikuwa Cyprus kama unavyosema lakini kikubwa ambacho kilinirudisha Tanzania ni pale mke wangu alipokaribia kujifungua, niliporudi tu baada ya muda nikaanza kuumwa sana na hivyo kushindwa kurudi Cyprus,” anasimulia.
 
“Tatizo hilo naweza kusema ni mambo yetu ya Kiswahili na ni huko Tanzania ndiyo kulikuwa chanzo, kuna vitu vilikuwa vinanitokea mwilini kiasi kwamba nilikuwa najikuna sana mwili mzima, hospitali nilikwenda na kupima vipimo vyote hakukuonekana kitu, kuna wakati wakaniambia ni fangasi.
 
“Nikaona hapana bora nigeukie upande wa pili wa tiba asilia, nako hali haikuwa rahisi nilizidi kuteseka ilifikia hatua najikuna mpaka vidonda vinatoka miguuni nikaona sasa na vidonda hivi nitarudije Cyprus bora nitibiwe kwanza kabla ya kuondoka.
 
“Ukweli ni kwamba nilizunguka sana kwa wataalamu mbalimbali kiu yangu ilikuwa ni kuhakikisha nakuwa sawa, nakumbuka mwanzoni kama ndani ya miezi miwili nilitumia hadi Sh6milioni kusaka tiba lakini bado ikashindikana, nilikuwa nataka kuhakikisha napona haraka ili niwahi kurudi kazini.
 
“Nilizunguka sana nakumbuka baada ya kuona Tanzania ni vigumu nikaondoka na kuja hapa Rwanda nako nilitibiwa hali haikuwa sawa, nikaenda DR Congo kidogo nikapata nafuu lakini baadaye kuna mtalaamu mmoja akanisaidia tena kwa kiasi kidogo maradhi yakapungua.
 
“Kuna mtu namjua kwamba alikuwa akifanya haya yote, hili nililiamini baada ya kumrudia Mungu, ukiacha ya Mungu pia hata hao wataalamu karibu wote nilipokuwa napita walikuwa wakimtaja sioni kama walikuwa wanadanganya kwani ni watu tofauti wote wamemtaja mtu mmoja, namuachia Mungu na nashukuru sasa nimeanza kurudi katika hali yangu.
 
“Baada ya misukosuko yote hiyo Baba yangu (Ndikumana Kitenge) kule nyumbani ana timu yake ndogo ya vijana, nikawa natumia muda huo kumsaidia majukumu ya kuwafundisha vijana na hapohapo na mimi nafanya mazoezi, nilipoona hali imeimarika nikaenda Vital’O kuwaomba nifanye nao kazi wakakubali na nashukuru walinielewa na kuniamini sasa nipo nao kwa muda.


“Sijasaini mkataba na Vital’O unajua kuna wakati  nafanya mazoezi kuna timu za Ulaya zilikuwa zinataka kunifuata nikaona niende Vital’O ili nijiweke sawa endapo watakuja wanikute katika hali nzuri lakini hao jamaa walivutiwa na mimi wakati nacheza kama beki na sasa hapa natumika kama kiungo mkabaji sijajua kama wakija watanikubali.”
 
Alikutana wapi na Uwoya?
“Unajua Irene nilimpenda kupitia filamu nilipomuona nikataka siku moja nikutane naye, nashukuru Mungu kuna siku wakati nataka kwenda Kigoma katika harusi ya dada yangu nilipitia Dar es Salaam nikakutana naye pale uwanja wa ndege.
 
“Sijabadili dini, ni kweli kwamba tulifunga ndoa ya kanisani lakini sikubadili dini nilitajwa kwa jina la Hamad Ndikumana, tulikubaliana na mke wangu tufunge ndoa mbili ya Kikristo na Kiislamu ikatangulia ile hii nyingine tukasema tutaifunga baadaye lakini muda ukawa mdogo ila tutaifunga hakuna shida.
 
Ni kweli wameachana na Uwoya?
“Kwanza nashangaa hao wanaodai nimeachana na mke wangu wanajua nani amempa talaka mwenzake? Sijaachana na Uwoya, yule ni mke wangu isipokuwa kwa sasa ni kama tumetengana na huko si kuachana labda watu wanachanganya mambo.
 
“Kuna mambo tulishindwa kukubaliana, alikuwa hataki kuja kuishi na mimi kule Cyprus, alikuwa anataka tuishi Tanzania tu, sasa mimi kazi yangu ni soka siwezi kuacha kazi ili nirudi Tanzania niishi na familia yangu bila ya kuwa na kazi hilo lilitufanya tutengane kidogo.
 
“Achana na mtoto nipo na maelewano mazuri na Uwoya hadi sasa tunawasiliana ngoja nikuthibitishie (Anainua simu na kumpigia lakini haipokelewi) nadhani atakuwa katika kazi zake, yupo safarini Afrika Kusini amekwenda kurekodi filamu na hata Krish ni mwanangu kila ninapotaka kumuona namuona bila shida.
 
“Sasa ana miaka mitatu na tumeshamwanzisha shule, anasoma (ananionyesha video fupi Krish aliyorekodiwa akihesabu namba kwa Kiingereza) nadhani sasa utaniamini unajua watu hawajui mimi na Irene ni wapenzi na tunaonana kila tunapopata nafasi.
 
“Hayo ni maneno ya watu tu, unajua Tanzania maneno ni mengi sana, kweli kuna wakati yanasemwa mengi sana ninaposikia nakutana na mwenzangu namuuliza anakataa lakini ukiacha kukataa kwake hata mimi nimeshindwa kuthibitisha hayo madai kwa hiyo nayaacha maisha yanaendelea.
 
“Kila kitu kina muda wake bado naamini siku moja nitarudi kuwa karibu na familia yangu, kwa sasa acha kwanza kila mmoja afanye yake ya kikazi, baadaye tutatulia na kuwa pamoja, watu waache kutugombanisha,”anasisitiza.

Chanzo:  Mwanaspoti

Baba amuingilia bintiye kinyume cha maumbile

Kanisa lawataka wachungaji wajiuzulu CHADEMA


Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Kusini ambaye pia ni Mchungaji wa Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT), Joseph Matare amejiuzulu nafasi yake hiyo kutokana na kanisa lake kuwataka wachungaji wake ambao ni viongozi wa vyama vya siasa kuachana na nafasi zao za kisiasa. 
 
Joseph Matare akizungumza na waandishi wa habari mjini Songea amesema kuwa ameamua kujiuzulu nafasi yake ya uongozi wa Chadema Kanda ya Kusini inayojumuisha mikoa ya Lindi, Mtwara na Ruvuma baada ya kanisa lake katika mkutano wake wa kanda kuagiza wachungaji wake ambao ni viongozi wa siasa kuachia nafasi zao na badala yake wasimamie kazi ya Mungu katika makanisa yao.
 
“Kufuatia maagizo ya mkutano huo wa kanisa uliofanyika Njombe nimeamua kutii... nimeamua kujiuzulu na katibu wangu mkuu, Dk Willibrod Slaa nilimjulisha tangu tarehe 4 Juni mwaka huu,” alisema Matare katika taarifa yake ya kujiuzulu.
 
Amefafanua kuwa muda wa viongozi wa kanda ulikuwa ni wa muda na wa mpito hadi uchaguzi wa kanda utakapopita ambao ulipaswa kufanyika Juni 2014 na kwamba muda umeongezwa hivyo ameona aheshimu maagizo yaliyomweka madarakani.
 
Hata hivyo, Matare anasema kuwa anawatia moyo makamanda wote wa Chadema waliobaki kuendelea kupigania nchi ili iondokane na uovu unaotendeka sasa na kwamba Mungu atakuwa nao wale wote wanaotafuta haki kwa ajili ya wananchi walio wengi.

Rais Kikwete: Uchaguzi Serikali za Mitaa kusogezwa mbele


RAIS Jakaya Kikwete amesema uchaguzi wa serikali za mitaa ambao ulikuwa ufanyike mwezi Oktoba mwaka huu, huenda ukasogezwa mbele kutokana na kutokamilika kwa mchakato wa rasimu ya mabadiliko ya Katiba.
 
Kauli hiyo ameitoa kwenye mkutano wa majumuisho ya ziara yake ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Tanga.
 
Alisema kulingana na hali ilivyo hivi sasa ambapo Bunge la Katiba halijakamilisha kazi zake, ni dhahiri kwamba uwezekano wa kufanyika kwa uchaguzi huo kwa kutumia Katiba mpya haupo.
 
“Kwa mfano, wabunge endapo wataamua wapitishe kwamba katiba itambue serikali 3 ni lazima kwanza itungwe katiba ya Tanganyika ambayo itaainisha taratibu zitakazotoa mwongozo wa uchaguzi…hata kama itabaki kama ilivyo …. bado muda wa kuandaa huo utaratibu wa uchaguzi wa serikali za mitaa hautatosha kwa sasa”, alisema.
 
Aidha aliongeza, “Nimeona niliseme hili japo kwa ufupi kwamba uchaguzi huu huenda utalazimika kusogezwa mbele kutokana na kutokamilika kwa mchakato wa Rasimu ya mabadiliko ya Katiba“, alisema.
 
Katika hatua nyingine, Rais amewataka Maofisa Kilimo kwenye halmashauri kujiendeleza kitaaluma na kuwa mabingwa waliojikita katika taaluma ya mazao yanayostawi kwenye maeneo yao badala ya kuyashughulikia kwa ujumla mazao yote yanayolimwa na wananchi.
 
Alisema utekelezaji wa agizo hilo utaongeza mavuno kwa zao husika, utapanua wigo wa uzalishaji pamoja na utaalamu katika kushughulikia zao, aina ya zao na kuleta tija katika sekta ya kilimo.
 
Alisema hatua ya maofisa kilimo kuendelea kujishughulisha kwa ujumla na mazao yote yanayostawi bila kuwa na lengo la kusimamia mazao maalumu, kunaifanya sekta hiyo kudumaa na hivyo kushindwa kuwakwamua kiuchumi wananchi.
 
“Nimegundua kwamba watu wetu wengi hawana utaalamu uliobobea…hata maofisa kilimo wetu hawana taaluma maalumu zilizojikita kwenye aina ya mazao mengine zaidi ya mpunga na mahindi, hatua ambayo inawasababisha washindwe kusimamia vizuri uzalishaji wa mazao mengine ambayo yangeweza kuwakwamua kiuchumi wakulima kwenye halmashauri husika,” alisema.
 
Aliongeza, “Kwa hiyo ni jukumu lenu viongozi wa halmashauri kuwachukua maofisa kilimo wenu na kuwapeleka SUA kwa ajili ya ku-specialize (kujikita) kulingana na vipaumbele vyenu vya mazao kwa sababu sio wote wanao ubingwa katika kila zao…tukifanikiwa kwenye hilo tutapata mafanikio zaidi”, alisema.
 
Aidha aliwataka viongozi kwenye mkoa wa Tanga kuhakikisha shughuli za kilimo zinajikita kwenye uzalishaji endelevu wa mazao ya matunda na mboga, kwa kuwa mkoa huo uko katika fursa nzuri kiuzalishaji zaidi ya mazao ya nafaka.

Dayna Nyange asimulia jinsi anavyoshambuliwa na Mashabiki kwa Lugha Chafu baada ya kuamua Kujichubua


Mwimbaji wa kike Dayna Nyange amezungumzia jinsi alivyokutana na changamoto nyingi baada ya kuamua kubadili rangi ya  ngozi yake na kuwa nyeupe.
 
Akiongea katika The Jump Off ya 100.5 Times Fm, Dayna ameeleza kuwa amekuwa akikosolewa na watu wengi huku wengine wakitumia lugha mbaya dhidi yake lakini yeye ameipokea vizuri kwa kuwa anaamini ni watu wanaompenda.
 
“Ni sawa kwa sababu mimi naamini ni watu wangu wa karibu na ni watu ambao wananipenda ndio maana wanakuwa wanasema japo wengine wanatumia kauli mbaya. Lakini pia ni sawa kwa sababu mimi najua hao ni binadamu na kila binadamu anajua jinsi ya kupresent kwa mtu vile ambavyo anajisikia kwa hiyo ni mimi kutumia tu akili nakipokeaje.” Amesema Dayna Nyange.
 
Ameeleza kuwa yeye anaamini hakuna kitu ambacho aliwahi kukifanya kabla kikawa gumzo au tatizo kwa watu na ndio maana watu wanaamua kulichukulia hili kama tatizo kubwa.
 
Mwimbaji huyo alitangaza uamuzi aliouchukua kufuatia changamoto hizo alizokutana nazo ingawa anaamini kila mtu anauhuru wa kufanya maamuzi kama alivyoamua yeye.
 
“Kwa hiyo mimi naweza kusema ni sawa, inawezekana kweli nimekosa. Lakini mimi kama binadamu pia nina maamuzi yangu na nina sababu nyingi tu za kufanya kile ninachokifanya. Japo nimesikia maneno mengi sana mpaka Lol..’nimeacha.!
 
“Siwezi kusema kuwa nimeacha kabisa lakini nimetoka kule nilikokuwa, sasa hivi narudi kuwa Dayna yule ambaye mnataka awe. Japo pia binadamu pia mnakitu kimoja, sifieni kile kilicho bora kabla hakijakuwa sio.” Ameaongeza.

Rose Ndauka Amkimbia Mumewe


Staa wa filamu za Kibongo, Rose Ndauka hivi karibuni aliamua kumkimbia mumewe Malick Bandawe, kisa mfungo wa Ramadhani ambapo sasa anaishi Kigogo na mama yake mzazi. 

Akipiga stori na mwanahabari wetu, Rose alisema amelazimika kwenda nyumbani kwao ili kumpisha mumewe atimize nguzo hiyo ya Uislam bila kipingamizi kutokana na kutokufunga ndoa.
 
“Mimi sifungi hivyo nimeona pia ni jambo la busara kumpa nafasi mwenzangu kwa ajili ya kufanya ibada hiyo, mwezi ukiisha nitarudi na maisha yetu yataendelea kama kawaida,” alisema Rose ambaye awali alikuwa akiishi na mumewe huyo Tandale jijini Dar.

Mwanamke Aliyemng'ata Hausigeli na kumchoma Pasi Aachiwa


Mtuhumiwa wa kesi ya kujeruhi kwa kumng'ata sehemu mbalimbali za mwili  mfanyakazi wa ndani, inayomkabili Amina Maige (42) amepatiwa dhamana jana baada  ya mahakama kuthibitisha kuwa hasira kutoka kwa wananchi zimepungua.
 
Hakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni, Yohana Yongolo alisema ameridhishwa na ufafanuzi uliotolewa na Mwendesha mashitaka wa Serikali pamoja na Wakili wa mshitakiwa kuwa haki ya dhamana itolewe kwa kufuata masharti na kwamba hakuna uhalifu wowote utakaofanyika dhidi ya mshitakiwa huyo.
 
Hakimu  Yongolo alitoa masharti ya dhamana ambayo yalimtaka Maige kutoondoka nje ya Dar es salaam bila ya ruhusa ya mahakama hiyo.
 
Pia alitoa masharti ya kuwa na wadhamini wawili wa kuaminiwa kutoka taasisi inayotambulika hapa nchini ambapo mdhamini huyo anaweza kuwa mwajiriwa, mfanya biashara na mkulima.
 
Alisema wadhamini hao watatakiwa kusaini hati ya makubaliano kwa kila mmoja kulipa Sh milioni tatu.
 
Aliongeza kuwa kesi hiyo itasikilizwa Julai 22 mwaka huu.
 
Maige alidaiwa Januari mwaka jana hadi Juni mwaka huu, alimng'ata na kumchoma na  pasi  sehemu mbalimbali za mwili wa  mfanyakazi waje wa ndani Yusta Kashinde (20) na kumsababishia maumivu mwilini.

Mbio za Urais 2015: Fredrick Sumaye Asema yeye ndo Tumaini pekee la Watanzania


WAZIRI Mkuu Mstaafu, Fredrick Sumaye, amesema yeye ni tumaini la Watanzania na mpambanaji wa vita dhidi ya maovu.
 
Kutokana na hali hiyo, amesema ni jemadari hodari aliyeungana na askari wapiganaji hodari wa vita ambao wataleta ushindi usio na shaka.
 
Kauli hiyo aliitoa jijini Mwanza jana, katika hotuba yake ya uzinduzi wa taasisi ya Vijana ya Tanzania Youth (TYDC), ambako alipinga hatua ya baadhi ya wanasiasa kununua wapiga kura kwenye uchaguzi na kufanikisha kitendo hicho ni sawa na uroho wa  madaraka. 
 
Alisema hali hiyo ni hatari, kwani wanasiasa wa aina hiyo wanapaswa kuangaliwa kwa umakini wa hali ya juu, wanaweza kulisambaratisha Taifa.
 
Sumaye ni mmoja wa makada sita wa CCM waliopewa onyo kutokana na kile kilichoelezwa kuanza kampeni za kuwania urais kabla ya wakati.
 
Akizungumza na MTANZANIA baada ya uzinduzi wa taasisi hiyo, Sumaye alisema yupo tayari kugombea urais iwapo ataombwa kufanya hivyo.
 
Akijibu maswali kwa waandishi wa habari, alisema dhamira yake katika kujitosa kuwania urais ipo, lakini pale atakapoombwa kugombea.
 
“Nikiombwa kugombea urais nitagombea, hilo wala halina tatizo…na mjue kutangaza nia siyo kosa kwa mujibu wa kanuni za CCM, ila kosa ni kufanya kampeni kabla ya muda, wakati rais anapomaliza muda wake wagombea wengi hujitokeza kuwania nafasi hiyo, sasa hata mimi nikiombwa nitagombea,” alisema Sumaye.
 
Sumaye, anayetajwa kuwa miongoni mwa wanasiasa ndani ya CCM wanaotaka kuwania urais mwaka 2015, akizungumza katika uzinduzi huo wa TYDC, alisema kuna watu wamekuwa wakitumia nguvu ya fedha kusaka madaraka na kuwafananisha na watu wafupi wanalazimisha kupanda juu ya stuli ili waonekane mbele ya jamii kwa kutumia nguvu kubwa ya fedha.
 
Alisema watu hao ni hatari iwapo wakichaguliwa na kushuka juu ya stuli kwa vile hawataonekana tena kuwasaidia wananchi na kubainisha wamekuwa wakiwatumia vijana vibaya ili kukidhi malengo yao binafsi, yakiwemo ya kisiasa.
 
Katika kongamano hilo, Sumaye alitangaza kuwa mlezi wa vijana nchini na kuwaahidi maisha ya matumaini kwa miaka ijayo.
 
“Mimi nataka niwe mlezi wa vijana wa Tanzania nzima ili wawe na maisha ya matumaini. Ninyi vijana mtu akiwaleteeni hela chukueni kuleni halafu mnamchagua mwingine. Yaani hata Sumaye akileta msikatae hela, chukueni kuleni msimchague, maana mtu anayetumia nguvu ya fedha kusaka madaraka ya Serikali za Mitaa, udiwani, ubunge na hata urais huyo hafai na ni dhaifu,” alisema Sumaye, huku akieleza hakuja kwenye kongamano hilo kwa sababu za kisiasa.
 
Aliwaasa vijana wote, hususan waliopo masomoni wasidanganyike wala kutegemea kupata ajira za ofisini na kwamba wasiopata ajira wasikubali kutumiwa kisiasa, vijana watakaotumiwa watakuwa wamejiunga katika kundi la wala rushwa na wapokea rushwa, watakuwa wamejiunga kwenye kundi la mafisadi na la maangamizi kwa taifa.
 
Alisema kwamba vijana ni jeshi muhimu la taifa kwa maslahi ya taifa na wananchi wake na siyo jeshi la kuleta maafa katika jamii, hivyo atakuwa mlezi wa vijana kwa mambo yote na sifa anayoipenda ni mtu kuwa mzalendo wa kweli, kusimamia haki ya umma na siyo maslahi binafsi.
 
Alisema kwamba, hivi sasa Watanzania wanaelekea kwenye uchaguzi na fedha nyingi zinatembezwa kwa vijana ili watoa rushwa wachaguliwe katika nafasi wanazoomba na kudai siku hizi kumeibuka mtindo wa watoa fedha kuitwa wakarimu na wasiotoa kuhonga wao huitwa wachoyo.
 
“Mliponitaka niwe mlezi wenu nilikubali kwa sababu mimi ni mpambanaji wa vita dhidi ya matatizo na maovu hayo ambayo TYDC imeyaweka kama malengo yake makuu.
 
“Hivyo niliona nimepata wapiganaji wenzangu katika vita hii na kwa bahati nzuri wapiganaji wenyewe ni vijana ambao ni wengi, ni wenye nguvu na ndio wenye uchungu na nchi yao. 
"Mimi ninawaahidi kuwa mmempata jemadari hodari wa kuongoza vita hii na yeye jemadari amepata askari mashujaa wa kupigana vita hiyo,” alisema.
 
Alisema muunganiko huo wa wawili wa jemadari hodari na askari wapiganaji hodari wa vita utaleta ushindi usio na shaka.
 
“Kama unavyoambiwa wewe na wenzako wengine wasiokuwa na mahesabu nao huambiwa vivyo hivyo. Lakini la msingi ujue kuwa kama mtu anatumia njia hizo za mkato kutaka kuingia madarakani, huyo mtu hajiamini na wala hana uhakika na uwezo wake wa kumudu hayo madaraka anayoyatafuta, vinginevyo asingehangaika kuhonga watu,” alisema Sumaye.
 
Awali akimkaribisha Sumaye kuzungumza na halaiki ya vijana zaidi ya 300, Mwenyekiti wa TYDC, Lengai Thomas Ole Sabaya, alionekana wazi kumpigia ‘debe’ Sumaye katika harakati zake za kisiasa, kwa kusema wakati wa utawala wake na Mkapa fedha ya Tanzania ilikuwa na thamani kuliko ilivyo leo hii.
 
Sumaye alikuwa Waziri Mkuu kwa miaka 10 katika Serikali ya Rais Benjamin Mkapa.
Februari 18, mwaka huu, Chama Cha Mapinduzi (CCM), kupitia Kamati Ndogo ya Udhibiti na Nidhamu katika kikao chake ilipendekeza kuchukuliwa hatua za kinidhamu kwa makada wake ambao wameanza kampeni ya kuwania urais wa mwaka 2015.
 
Uamuzi huo wa kamati hiyo ya maadili ulibarikiwa na Kamati Kuu (CC) ya CCM, iliyokutana Februari 17, mwaka huu mjini Dodoma, chini ya Mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete.
 
Makada waliopewa adhabu ya mwaka mmoja kwa tuhuma za kuanza kampeni za kuwania urais kabla ya wakati ni January Makamba, Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa, Waziri Mkuu Mstaafu Frederick Sumaye, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe.
 
Wengine ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu) Steven Wassira pamoja na aliyewahi kuwa Waziri wa Nishati na Madini ambaye ni Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja.
 
Katika adhabu hiyo, makada hao walizuiwa kujihusisha na masuala ya kisiasa ndani ya chama hicho kwa miezi 12, huku mwenendo wao wa kisiasa ukifuatiliwa chini ya uangalizi mkali katika kipindi chote cha kutumikia adhabu hiyo.
 
Kabla ya adhabu hiyo, makada hao waliitwa na kuhojiwa na Kamati Ndogo ya Maadili ambayo iliwatia hatiani kwa kutumia Kitabu cha Kanuni ya Uongozi na Maadili ya CCM, toleo la Februari 2010, Ibara 6 (7)(i).

Credit: Mtanzania

VJ Penny Achumbiwa.....Sasa kuanza Maisha Mapya baada ya kutemana na Diamond


Mtangazaji maarufu nchini VJ Penny ambaye alikuwa mpenzi wa Diamond Platnumz amechumbiwa.  Kupitia Instagram Penny ameweka picha akiwa amevaa pete ya uchumba  na  kuandika  ujumbe  huu: “Road trip ….site her we come…cc @halimakimwana1.” 
Pia juzi  tulisikia   kuwa Penny amechumbiwa ingawa hatukupata habari kwa kina mpaka Penny mwenyewe alipoweka picha Instagram  akiwa  amevaa  pete  ya  Uchumba.

VJ Penny ambaye  inadaiwa alikuwa chaguo la kwanza la mama Diamond Platinumz ameweka picha hiyo siku moja baada ya Wema Sepetu kupost picha nyingi kwenye Instagram akiwa na mama Diamond kwenye sherehe ya siku yake ya kuzaliwa na kuzipa caption mbalimbali huku nyingine zikiwa na vijembe.
Tunampa hongera zote VJ Penny kwa  kuchumbiwa.

Hii ni Aina Mpya ya Uhalifu wa Kimtandao inayokuja kwa Kasi nchini Tanzania


Miongoni mwa makosa yanayofanyika  mtandaoni  ni hili  lijulikanalo kama “Phishing” ambapo kosa hili limekuwa likidumu na  kukua  kwa  kasi  sana  katika nchi mbali mbali.

Nchi mbali mbali zimechukulia uhalifu huu kuwa ni hatari kwani unaweza kuwa na madhara makubwa kwa mtendewa ikiwa ni pamoja na kupelekea kumfilisi mtu, kupata taarifa za watu kinyume na sheria au makubaliano na hata wakati mwingine kupelekea kuleta madhara mengine kama kutumika kuhatarisha mifumo mbali mbali.

Kwa kuzingatia hili nchi mbalimbali zimekuwa na sheria kali dhidi ya uhalifu huu , huku nchi za afrika kupitia umoja wa wataalam wa maswala ya usalama mtandaoni wamekubalina  kuanzisha kamati yenye watu maalaum itakayoangazia macho uhalifu huu na kutoa taarifa huku hatua zikichukuliwa.

Makampuni ya Ati-vurus nayo yametoa uzito kwenye hili na kuhakikisha  wanaunda nyezo madhubuti za utambuzi wa aina hii ya uhalifu na mara kwa mara wakiwasilisha ripoti zao.
 
Changamoto bado zipo kutokana na upungufu wa uelewa kwa wananchi mbali mbali juu ya uhalifu huu inayo sababisha  waathirika kueendelea kuwa wengi kila kukicha.

Uchunguzi umeonyesha mara nyingi panapokuwa na jambo linalo fuatiliwa na wengi, wahalifu  nao  hujipenyeza hapo na kuanza kusambaza aina hii ya uhalifu.

Kwa upande wa Tanzania, Serikali  imekuwa  ikizungumza  mara  nyingi    na  kutoa  tahadhari  mbalimbali  juu  ya  uharifu  wa  kimtandao.

Ni vizuri tukakumbushana kuwa  Tanzania imesha kamilisha rasimu ya sheria za mitandao ambazo zitatoa fursa kwa wahalifu kushughulikiwa ipasavyo na hivi karibuni TCRA nayo ilizungumzia mpango wake wa kushughulikia watumiaji vibaya wa mitandao. Hili likiwa linafuatia kampeni yao ya Futa delete kabisa.

Wakati hili linajiri, kumekuwepoa na wimbi la wahalifu wa uhalifu huu wa "Phishing" ambao   hudukua na kuchukua akauti za mitandao za watu na kuanza kusambaza taarifa zitakazo wawezesha kupata taarifa za  wengine na mara nyingine wanatengeneza akaunti feki za mitandao wakitumia majina ya watu maarufu na kuanza kuzitumia vibaya.

Waharifu  hao  wamekuwa  wakitumia majina ya watu mashuhuri na kutumia watu ujumbe wakiwataka wabonyeze link ili kujiunga na huduma kama Vikoba, Pia wamekua wakituma ujumbe wakiwataka watu wafungue tovuti n.k

TAHADHARI: Kila mmoja anapaswa kuwa makini na unapo hisi ya kuwa unaweza ukawa muathirika wa uhalifu  wa  huu kimtandao basi badilisha neno la siri na siku zote jiepushe kujibu au kufuata maelekezo yatakayo kutaka ufanye kitu Fulani.

Jamaa anusurika Kunyofolewa Jicho baada ya kufumaniwa akingonoka na Mke wa Mtu ......Alivizia mwenye mke kasafiri, akazama Chumbani


Mkazi wa Mtaa wa Lagos, Wazo Mivumoni, Msitu wa Pande jijini Dar es Salaam, Nuru Makala ‘Baba Eliza’ (42) Jumatano iliyopita alikumbwa na majanga baada ya mwanaume aliyejulikana kwa jina la Yusuf Ally ‘Mgosi wa Ndima’ kudai amemfumania Baba Eliza akiwa na mkewe ambaye jina halikupatikana.

Tafrani hiyo ilijiri usiku wa Jumatano iliyopita, Juni 18, mwaka huu kwenye nyumba yake iliyopo Mtaa wa Lagos, Msitu wa Pande.
Akizungumzia  tukio  hilo  mbele  ya  wanahabari  waliokuwa  eneo  hilo  wakisaka  habari, Yusuf  Ally  ambaye  ni  mume  wa  mwanamke  aliyefumaniwa  alisema:
 
“Nilikuwa katika harakati za kumchunguza mke wangu kinyemela kwa siku nyingi kama anachepuka, nikabaini kuna mawasiliano yenye shaka kati yake na huyo jirani yangu.

“Nilipomuuliza mke wangu alikiri, akasema amekuwa akimwambia jirani yangu kwamba haiwezekani lakini jamaa anakomaa tu anamwambia wakutane, tena wakutane humu ndani.
 
“Ndipo nilipoamua kumuandaa mke wangu kwa mtego amwambie jamaa kuwa leo (siku ya tukio) sitakuwepo na sitarudi ili kumpa nafasi jamaa kuja kujinafasi. Baada ya kukamilisha mtego niliwasiliana na kamanda wa sungusungu wa eneo hilo, Kapteni Makumba na kumuelezea kinagaubaga.

“Kapteni Makumba aliwaandaa vijana wake ambapo kuanzia mishale ya saa mbili usiku walijibanza kwenye kichaka kilichopo mbele ya nyumba huku akifanya mawasiliano na mimi.”
 
Mgoni  akiomba  Msamaha.

Yusuf aliendelea kudai kuwa, ilipotimu saa tano usiku kukiwa kumetulia, Baba Eliza alionekana akikaribia nyumba ya jirani yake huyo kwa hatua za kunyata na kuangalia kulia na kushoto kisha akazama ndani huku mkononi akiwa ameshika kifurushi kilichobainika baadaye kwamba kilikuwa na machungwa kadhaa.

Alisema muda mfupi baada ya kuingia, sungusungu mmoja alikwenda kujibanza kwenye dirisha la chumba na kupiga chabo kilichokuwa kikiendelea ambapo alimshuhudia Baba Eliza akichojoa nguo chapchapu tayari kwa mtanange, sungusungu huyo akawatonya wenzake.
 
Yusuf akazidi kusema kwamba wote walitoka kichakani na kwenda kuvamia chumbani ambapo walimkuta mkewe aliyekuwa bado hajaanza kuvua nguo kwa sababu alijua majanga yatatokea muda si mrefu akiwa anajiandaa kufanya hivyo kiaina.

Baada ya hali kuwa shwari, Kamanda wa Sungusungu, Kapteni Makumba alianza kumsomea mashitaka jirani huyo aliyekuwa mtupu muda huo mbaye hakuwa na la kusema zaidi ya kuomba radhi na kumtupia lawama ibilisi kwamba ndiye aliyemshawishi na haikuwa amri yake.
 
Raia aliyeshuhudia mkasa huo akionesha sehemu ya kitanda  iliyochafuliwa na mgoni kwa kinyesi.
 
Sungusungu walimtaka Baba Eliza kumlipa fidia ya shilingi milioni moja mwenye mke kwa kitendo cha kumdhalilishia ndoa yake.

Source:  Ijumaa  Wikienda/ GPL

Kondomu zakutwa kwenye ukumbi wa bunge


Inaweza kuonekana ni kituko cha aina yake, lakini ni kweli kimetokea kwenye Ukumbi wa Bunge la Kaunti ya Nairobi na kuwaacha wabunge vinywa wazi. 
 
Katika hali isiyo ya kawaida, boksi la kondomu lilikutwa ndani ya ukumbi huo na kuwashtua wabunge wote akiwamo spika wa bunge hilo.
 
Mwakilishi wa eneo la Karura, Kamau Thuo ndiye aliyekuwa wa kwanza kuliona boksi hilo na kuwashtua wabunge wengine hali iliyoibua mjadala mzito.
 
Kutokana na sintofahamu hiyo Spika Alex Ole Magelo aliwataka wahudumu kufungua boksi hilo kujua kilichomo ndani yake ndipo walipokuta kondomu.
 
“Nafahamu wote humu ni watu wazima, lakini ninachoshangaa ni nani ambaye ameleta kondomu hizi ndani ya ukumbi huu,” alihoji Spika Magelo.
 
Hata hivyo, Mwenyekiti wa Kamati ya Afya, Manoah Mboku aliwaondoa hofu wabunge na kueleza kuwa kondomu hizo zilipaswa kuwekwa kwenye vyoo vya wanaume hata hivyo kwa bahati mbaya zikapelekwa mahali kusikohusika.

TOBA ANGALIA PICHA ZA MKE WA BOSS ALIVYONASWA AKILIWA KIBOGA NA HOUSE BOY WAO AIBU KUBWA ANGALIA PICHA TUKIO ZIMA...!


Zamani tulikuwa na hofu na mahouse girl kuvunja ndoa za watu lakini kwa sasa mabo yamebadilika.Kiongozi mkubwa mstaafu serikalini (Mr Kelechi) ameshangazwa na kile kinachoitwa sintofahamu baada ya kuona maajabu kwenye simu ya mfanyakazi wake wakiume wa nyumbani kwake(house boy).

Taarifa zinasema kiongozi huyo alichukua simu ya mfanyakazi wake iliafanye mawasiliano
lakini katika kuichezea alizikuta picha za uch za mke wake.Mapigo ya moyo yalibadilika, ndugu msomaji usiombe uibiwe mke ni bora ukaibiwa hata pesa.

WATU WAZIDI KUMSHAMBULIA FROLA MBASHA, KUMBE MDOGO WAKE ANAYEDAIWA KUBAKWA NDO ALIREKODIWA AKIFANYA MAPENZI NA NGASA???

Copy paste by Coco master. Hili suala naliwaza sn nahisi kuna kitu nyuma ya pazia isijekua Mali mlizochuma zikasababisha kumpoteza mmoja Kwa style hii . Binafsi kuhusu suala la Mbasha sidhani na siamini kama alibaka ila tabia ya mdogo wa Frola Mbasha si nzuri, alishawahi kuonekana kwenye magazeti na video yake ya ngono aliyoicheza na mchezaji maarufu Tanzania, Sasa kama yule mchezaji hakuchukuliwa hatua yeyote ilihali huyu binti alikuwa mwanafunzi na alitoroka shule, basi Mbasha hastahili kuwa hatiani, nimemshangaa sana dada Yangu Frola Mbasha kwa kwenda kwenye Television na kumuaibisha mume wake akisahau kuwa yeye ni ubavu tena wakushoto na anayemuaibisha ni mume wake na wamebahatika kupata mtoto,maandiko yameandika mwanamke atawaacha wazazi wake na kumfuata mumewe, pia kilichounganishwa na MUNGU kamwe hakuna atakayeweza kukitengua ina maana hamkuunganishwa na MUNGU?, mdogo wako ni pornstar na wewe unafahamu, kwanini umpe ukaribu na mumeo?sumu hawaonji kwa kuilamba? Tubu msamehe mwenzio, hayo yote yanapita na maisha yanaendelea!

WAJUE WANAUME ZAIDI YA 15 WALIOWAHI KUMFAIDI KIM KARDASHIAN…

Vitu ambavyo watu wanavifanya chumbani ni siri yako na mwezi wako lakini mara nyingi  unapokua maarufu basi vitu hivi sio siri tena.Hivi sasa kim ameshaolewa na bwana Kanye lakini mikasa aliyoipata katika maisha yake ya mapenzi ndio imetufanyavibe Tanzania kuangalia kwa jicho la pili mahusiano aliyopitia bibie Kim Kardashian.Akiwa tayari ana miaka 31 , Kim amepitiwa na wanaume wengi huku wengine wakiwa ni mpango wa kando wakati tayari ana mtu mwingine. Hii ni list ya wanaume  (wanaojulikana na maarufu)ambao wameshawai kumpitia kim tokea mwaka 1994 :-
Kim-Kardashian-Featured
TJ Jackson (1994-1998)
katika interview yake na Oprah, Kim alisema alianza kutumia njia za uzazi akiwa na miaka 14 ambapo alikua ataki kushika mimba akiwa na mdogo. TJ Jackson kama ulikua hujui, huyu ni mpwa “nephew” wa Michael Jackson ambapo inasemekana ndio alikua sio tu wa kwanza kutoka naye bali wa kwanza pia kufanya naye mapenzi.
TJ-Jackson-Kim-Kardashian
Damon Thomas (2000-2004)
Unafikiri kim hakuwahi kuolewa kabla? basi kama ndio , habari ni kwamba kim akiwa na umri wa miaka 20 aliolewa na producer , Damon Thomas , ndoa iliyodumu kwa miaka minne tokea mwaka 2000 hadi mwaka 2004. Ndoa yao ilivunjika kutokana na kim kupigwa mingumi na mwanaume huyu . Pia Kim alikua akifuatiliwa kila dakika anapopumua.
Kim-Kardashian-and-Damon-Thomas
Julian St. Jox (2001)
Huyu Jamaa ambaye ni muigizaji wa muvi za kikubwa (pornstar) ambaye  alimmaliza kim wakati kim akiwa yupo kwenye ndoa katika party moja waliokua nae. Julian alisema kim alitokea katika  hoteli ya Wyndham na mwanaume mweusi ambae anahisi alikua mme wake kipindi hicho, Damon ambapo alimfuata kim huku akiwa na pornstar mwenzake wa kike Emily Ann ambapo walianza kucheza na mizuka kupanda ambapo watatu hao walitafuta chumba na mengine yakabaki kua story.
Julian-St-Jox--Kim-Kardashian
Ray J (2002 – 2003)
Hivi kunaaja ya kuielezea hii kitu ? kwa wale wanaopenda picha za ngono , mtakua mmeshaona mkanda wa ngono kati ya Ray J na Kim Kardashian uliovuja. Kipindi mkanda huo unarekodiwa , Kim Kardashian alikua bado yupo kwenye ndoa yake na Damon. Duh! jamaa alikua bwege kweli…Kumbuka mkanda huu wa ngono ulivuja mwaka 2007 japokua ulirekodiwa mwaka 2003. Kama ulikua hujui mwaka 2007 ndio ulikua mwanzo wa kipindi cha Keeping up with the kardashians na wataalamu wanasema kipindi hiki kililenga kumsafisha kim bila kujua mafanikio ambayo kingepata.
Kim-KArdashian-and-Ray-J
Nick Lachey (2006)
Mwanamuziki huyu kutoka bendi ya 98 Degrees alitoka na Kim Kardashian kwa wiki moja tu na mahusiano yake yakavunjika. Nick alikua ametoka kuvunja ndoa yake na mwanamuziki Jessica Simpson na muda mchache akaanza kutoka na kim. Nick anadai Kim alimtumia kujipatia umaarafu baada ya kusema kim aliwalipa mapaparazi zaidi ya 30 kumpiga picha walipokua wanatoka movies. Nick anasema picha zake kati yake na Kim ndio ulikua mwanzo wa mafanikio ya Kim.
Nick-Lachey-and-Kim-Kardashian

Nick Cannon (September 2006- January 2007)
Hehehe, unajua kwanini Nick Cannon alimtosa Kim kardashian ? wapenzi hawa walikua wakiishi vizuri hadi pale Kim alipoulizwa na Nick kuhusu kuwepo kwa mkanda wa ngono kati yake na Ray J na Kim kumdanganya na kumwambia hamna kitu kama hicho. Nick alisema hataweza kumsamehe Kim kwa uwongo aliyomwambia.
Nick-Cannon-and-Kim-Kardashian
 Reggie Bush (2007)
Huyu ni mchezaji wa mpira (NFL) wa marekani ambae alikua na mahusiano na kim kwa zaidi ya miaka miwili hadi mwaka 2009 lakini mahusiano yao yalikua yakutosana na kurudiana baadae.
reggie-Bush-and-Kim-KArdashian
Evan Ross (2007)

Huyu ni mtoto wa mwanamuziki wa zamani na maarufu kabisa nchini marekani, Diana Ross. Wawili hawa walitoka pamoja kipindi kardashian alipuamua kupumzisha penzi la Reggie Bush.
Evans-Ross-and-Kim-Kardashian
Christiano Ronaldo (April 2010)
Hiki kipindi mrembo Kim alikua nchini Hispania kimapumziko ndipo alipokutana na Christiano Ronaldo. Kipindi hicho christiano akiwa na miaka 25 huku Kim akiwa na 29 , wawili hao walionekana kwa mara ya kwanza wakipeana mahaba ndani ya siku 3 ambazo kim alikua nchini humo.
Christiano-Ronaldo-Kim-Kardashian
Shengo Deane (April 2010)
katika interview yake ya Piers Morgan kim alieleza jinsi alivyohuzunika kuhusu sex tape yake ya mwaka 2007 lakini chaushangaza aliweza kuonyesha mahaba yake na Shengo Deane katika kipindi cha keeping up with the Kardshians. Kumbuka mu-Australia huyu alikua ni bodyguard wa Kim Kardashian.
Shengo-Deane-and-Kim-Kardashian
Miles Austin (June 2010)
Huyu naye ni mchezaji wa American Football. Wawili haya walidumu kwa miezi na hakuna sababu ya msingi ya kutengana kwao zaidi ya long distance.
Miles-Austin-and-Kim-KArdashian
Michael Copon (October 2010)
huyu ni muigizaji aliyemjua Kim kwa zaidi ya miaka 11 na baadae wakafanya yao japokua uhusiano wao haukudumu kabisa kwa alichokisema Michael kwamba Kim anatabia za kitoto.
Michael-Copon-and-Kim-Kardashian
John Mayer (October 2010)
Hii ilikua mwishoni mwa mwezi October ambapo kim aliamua isiwe tabu na kumuachia mwanamuziki na producer , John Mayer ale mema ya nchi
Jon-Mayer--and-Kim-Kardashian
Gabriel Aubrey (November 2010)
Huyu ni model kutoka nchini Canada na kipindi anatoka na Kardashian alikua ana mtoto wa miaka miwili aliyezaa na msanii Halley Berry.
Gabriel-Aubrey-and-Kim-Kardashian
Kris Humphries (2010-2013)
Hii ilikua ndoa ya pili kwa kim Kardashian. Hii ndoa kati ya Kris Humphries na Kim Kardashian ni maarufu kwasababu iliweza kudumu kwa siku 72 tu ! Ndoa ya mcheza kikapu huyu wa NBA na Kim ilifika mwisho baada ya Kim kuhisi kwamba hamna jema litakalotokea baadae na Kris pia kuhisi Kim anachepuka kwa rapper Kanye West.
kris-humphries-and-kim-kardashian
Kanye West (2007 hadi leo)
Unashangaa nini sasa ? Kim Kardashian alikua akichepuka kwa Kanye kipindi ana mahusiano na Reggie Bush na Kris Humpries.Kwasasa Kim na Kanye ni wanandoa na wanamtot mmoja, North West.
Kim-Kardashian-And-Kanye-West
Duh, hivi kwa hii list wewe ungekubali kumuoa Kim kwa mara ya tatu kama alivyofanya kanye tena ukizingatia kuna wengine waliopita sema bila uhakika kama 50cent, The Game, Brett Lockett, Scot Storch  na wenine wasio celebrities ?