Hii ni Aina Mpya ya Uhalifu wa Kimtandao inayokuja kwa Kasi nchini Tanzania


Miongoni mwa makosa yanayofanyika  mtandaoni  ni hili  lijulikanalo kama “Phishing” ambapo kosa hili limekuwa likidumu na  kukua  kwa  kasi  sana  katika nchi mbali mbali.

Nchi mbali mbali zimechukulia uhalifu huu kuwa ni hatari kwani unaweza kuwa na madhara makubwa kwa mtendewa ikiwa ni pamoja na kupelekea kumfilisi mtu, kupata taarifa za watu kinyume na sheria au makubaliano na hata wakati mwingine kupelekea kuleta madhara mengine kama kutumika kuhatarisha mifumo mbali mbali.

Kwa kuzingatia hili nchi mbalimbali zimekuwa na sheria kali dhidi ya uhalifu huu , huku nchi za afrika kupitia umoja wa wataalam wa maswala ya usalama mtandaoni wamekubalina  kuanzisha kamati yenye watu maalaum itakayoangazia macho uhalifu huu na kutoa taarifa huku hatua zikichukuliwa.

Makampuni ya Ati-vurus nayo yametoa uzito kwenye hili na kuhakikisha  wanaunda nyezo madhubuti za utambuzi wa aina hii ya uhalifu na mara kwa mara wakiwasilisha ripoti zao.
 
Changamoto bado zipo kutokana na upungufu wa uelewa kwa wananchi mbali mbali juu ya uhalifu huu inayo sababisha  waathirika kueendelea kuwa wengi kila kukicha.

Uchunguzi umeonyesha mara nyingi panapokuwa na jambo linalo fuatiliwa na wengi, wahalifu  nao  hujipenyeza hapo na kuanza kusambaza aina hii ya uhalifu.

Kwa upande wa Tanzania, Serikali  imekuwa  ikizungumza  mara  nyingi    na  kutoa  tahadhari  mbalimbali  juu  ya  uharifu  wa  kimtandao.

Ni vizuri tukakumbushana kuwa  Tanzania imesha kamilisha rasimu ya sheria za mitandao ambazo zitatoa fursa kwa wahalifu kushughulikiwa ipasavyo na hivi karibuni TCRA nayo ilizungumzia mpango wake wa kushughulikia watumiaji vibaya wa mitandao. Hili likiwa linafuatia kampeni yao ya Futa delete kabisa.

Wakati hili linajiri, kumekuwepoa na wimbi la wahalifu wa uhalifu huu wa "Phishing" ambao   hudukua na kuchukua akauti za mitandao za watu na kuanza kusambaza taarifa zitakazo wawezesha kupata taarifa za  wengine na mara nyingine wanatengeneza akaunti feki za mitandao wakitumia majina ya watu maarufu na kuanza kuzitumia vibaya.

Waharifu  hao  wamekuwa  wakitumia majina ya watu mashuhuri na kutumia watu ujumbe wakiwataka wabonyeze link ili kujiunga na huduma kama Vikoba, Pia wamekua wakituma ujumbe wakiwataka watu wafungue tovuti n.k

TAHADHARI: Kila mmoja anapaswa kuwa makini na unapo hisi ya kuwa unaweza ukawa muathirika wa uhalifu  wa  huu kimtandao basi badilisha neno la siri na siku zote jiepushe kujibu au kufuata maelekezo yatakayo kutaka ufanye kitu Fulani.