Trafiki Anusurika kufa baada ya Kuvaana Uso kwa Uso na Gari Dogo eneo la Bamaga Mikocheni jijini Dar es salaam


Askari mmoja wa kikosi cha usalama barabara ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja amenusurika kufa baada ya kupata ajali akiwa anaendesha pikipiki ya polisi ambayo ilikosa mwelekeo na kugongana uso kwa uso na gari dogo lenye namba za usajili T 681 CUX eneo la Bamaga Mikocheni jijini Dar es salaam ambapo gari hilo lilikuwa likiandeshwa na mwanamke mmoja huku mashuhuda wa ajali hiyo kila mmoja akiwa na mtazamo tofauti juu ya ajali hiyo.

Irene Uwoya amtaka Ndikumana Yanga, mwenyewe aogopa kulogwa.....Asema Uwoya bado ni Mke wake na wanapendana sana


BINTI aliyejaliwa uzuri wa sura anayeng’ara kwenye filamu za Kibongo, anamshawishi mumewe Hamad Ndikumana aje kucheza Yanga ya chini ya kocha, Marcio Maximo.
 
Ndikumana ambaye kwa sasa anaichezea Vital’o ya Bujumbura, Burundi ameweka wazi kwamba binti huyo, Irene Uwoya ambaye ni mkewe ni shabiki wa Jangwani na amekua akimshawishi kila mara kwamba atue Jangwani ili awe naye karibu zaidi kwani hana mpango wa kuondoka Dar es Salaam kwenye kazi zake za filamu.
 
Mchezaji huyo amekiri kushawishiwa mara nyingi lakini alisema hawezi kujipeleka Yanga mpaka timu hiyo itakapomfuata, kama hiyo haitoshi aliongeza kwamba anaogopa kuishi Dar es Salaam kutokana na mambo ya ushirikina yaliyomtokea alipoanza maisha na mkewe ambaye ameshangaa watu wanaozusha kwamba wameachana.
 
“Ananitaka nije kucheza Tanzania alikuwa ananiambia nije Yanga, unajua anaipenda sana Yanga lakini nikamwambia mimi ni mchezaji ninayejiamini siwezi kuja kuomba Yanga wanisajili acha waje wao tuzungumze, yuko tayari kufanya hata ushawishi kwa wadau,” anasisitiza Ndikumana ambaye awali alikuwa akiichezea APOP Kinyras Peyias ya Cyprus.
 
Ndikumana alisema kilichomtoa Cyprus na kuja Burundi pamoja na uhusiano wake na Uwoya.
 
“Kweli nilikuwa Cyprus kama unavyosema lakini kikubwa ambacho kilinirudisha Tanzania ni pale mke wangu alipokaribia kujifungua, niliporudi tu baada ya muda nikaanza kuumwa sana na hivyo kushindwa kurudi Cyprus,” anasimulia.
 
“Tatizo hilo naweza kusema ni mambo yetu ya Kiswahili na ni huko Tanzania ndiyo kulikuwa chanzo, kuna vitu vilikuwa vinanitokea mwilini kiasi kwamba nilikuwa najikuna sana mwili mzima, hospitali nilikwenda na kupima vipimo vyote hakukuonekana kitu, kuna wakati wakaniambia ni fangasi.
 
“Nikaona hapana bora nigeukie upande wa pili wa tiba asilia, nako hali haikuwa rahisi nilizidi kuteseka ilifikia hatua najikuna mpaka vidonda vinatoka miguuni nikaona sasa na vidonda hivi nitarudije Cyprus bora nitibiwe kwanza kabla ya kuondoka.
 
“Ukweli ni kwamba nilizunguka sana kwa wataalamu mbalimbali kiu yangu ilikuwa ni kuhakikisha nakuwa sawa, nakumbuka mwanzoni kama ndani ya miezi miwili nilitumia hadi Sh6milioni kusaka tiba lakini bado ikashindikana, nilikuwa nataka kuhakikisha napona haraka ili niwahi kurudi kazini.
 
“Nilizunguka sana nakumbuka baada ya kuona Tanzania ni vigumu nikaondoka na kuja hapa Rwanda nako nilitibiwa hali haikuwa sawa, nikaenda DR Congo kidogo nikapata nafuu lakini baadaye kuna mtalaamu mmoja akanisaidia tena kwa kiasi kidogo maradhi yakapungua.
 
“Kuna mtu namjua kwamba alikuwa akifanya haya yote, hili nililiamini baada ya kumrudia Mungu, ukiacha ya Mungu pia hata hao wataalamu karibu wote nilipokuwa napita walikuwa wakimtaja sioni kama walikuwa wanadanganya kwani ni watu tofauti wote wamemtaja mtu mmoja, namuachia Mungu na nashukuru sasa nimeanza kurudi katika hali yangu.
 
“Baada ya misukosuko yote hiyo Baba yangu (Ndikumana Kitenge) kule nyumbani ana timu yake ndogo ya vijana, nikawa natumia muda huo kumsaidia majukumu ya kuwafundisha vijana na hapohapo na mimi nafanya mazoezi, nilipoona hali imeimarika nikaenda Vital’O kuwaomba nifanye nao kazi wakakubali na nashukuru walinielewa na kuniamini sasa nipo nao kwa muda.


“Sijasaini mkataba na Vital’O unajua kuna wakati  nafanya mazoezi kuna timu za Ulaya zilikuwa zinataka kunifuata nikaona niende Vital’O ili nijiweke sawa endapo watakuja wanikute katika hali nzuri lakini hao jamaa walivutiwa na mimi wakati nacheza kama beki na sasa hapa natumika kama kiungo mkabaji sijajua kama wakija watanikubali.”
 
Alikutana wapi na Uwoya?
“Unajua Irene nilimpenda kupitia filamu nilipomuona nikataka siku moja nikutane naye, nashukuru Mungu kuna siku wakati nataka kwenda Kigoma katika harusi ya dada yangu nilipitia Dar es Salaam nikakutana naye pale uwanja wa ndege.
 
“Sijabadili dini, ni kweli kwamba tulifunga ndoa ya kanisani lakini sikubadili dini nilitajwa kwa jina la Hamad Ndikumana, tulikubaliana na mke wangu tufunge ndoa mbili ya Kikristo na Kiislamu ikatangulia ile hii nyingine tukasema tutaifunga baadaye lakini muda ukawa mdogo ila tutaifunga hakuna shida.
 
Ni kweli wameachana na Uwoya?
“Kwanza nashangaa hao wanaodai nimeachana na mke wangu wanajua nani amempa talaka mwenzake? Sijaachana na Uwoya, yule ni mke wangu isipokuwa kwa sasa ni kama tumetengana na huko si kuachana labda watu wanachanganya mambo.
 
“Kuna mambo tulishindwa kukubaliana, alikuwa hataki kuja kuishi na mimi kule Cyprus, alikuwa anataka tuishi Tanzania tu, sasa mimi kazi yangu ni soka siwezi kuacha kazi ili nirudi Tanzania niishi na familia yangu bila ya kuwa na kazi hilo lilitufanya tutengane kidogo.
 
“Achana na mtoto nipo na maelewano mazuri na Uwoya hadi sasa tunawasiliana ngoja nikuthibitishie (Anainua simu na kumpigia lakini haipokelewi) nadhani atakuwa katika kazi zake, yupo safarini Afrika Kusini amekwenda kurekodi filamu na hata Krish ni mwanangu kila ninapotaka kumuona namuona bila shida.
 
“Sasa ana miaka mitatu na tumeshamwanzisha shule, anasoma (ananionyesha video fupi Krish aliyorekodiwa akihesabu namba kwa Kiingereza) nadhani sasa utaniamini unajua watu hawajui mimi na Irene ni wapenzi na tunaonana kila tunapopata nafasi.
 
“Hayo ni maneno ya watu tu, unajua Tanzania maneno ni mengi sana, kweli kuna wakati yanasemwa mengi sana ninaposikia nakutana na mwenzangu namuuliza anakataa lakini ukiacha kukataa kwake hata mimi nimeshindwa kuthibitisha hayo madai kwa hiyo nayaacha maisha yanaendelea.
 
“Kila kitu kina muda wake bado naamini siku moja nitarudi kuwa karibu na familia yangu, kwa sasa acha kwanza kila mmoja afanye yake ya kikazi, baadaye tutatulia na kuwa pamoja, watu waache kutugombanisha,”anasisitiza.

Chanzo:  Mwanaspoti

Baba amuingilia bintiye kinyume cha maumbile

Kanisa lawataka wachungaji wajiuzulu CHADEMA


Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Kusini ambaye pia ni Mchungaji wa Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT), Joseph Matare amejiuzulu nafasi yake hiyo kutokana na kanisa lake kuwataka wachungaji wake ambao ni viongozi wa vyama vya siasa kuachana na nafasi zao za kisiasa. 
 
Joseph Matare akizungumza na waandishi wa habari mjini Songea amesema kuwa ameamua kujiuzulu nafasi yake ya uongozi wa Chadema Kanda ya Kusini inayojumuisha mikoa ya Lindi, Mtwara na Ruvuma baada ya kanisa lake katika mkutano wake wa kanda kuagiza wachungaji wake ambao ni viongozi wa siasa kuachia nafasi zao na badala yake wasimamie kazi ya Mungu katika makanisa yao.
 
“Kufuatia maagizo ya mkutano huo wa kanisa uliofanyika Njombe nimeamua kutii... nimeamua kujiuzulu na katibu wangu mkuu, Dk Willibrod Slaa nilimjulisha tangu tarehe 4 Juni mwaka huu,” alisema Matare katika taarifa yake ya kujiuzulu.
 
Amefafanua kuwa muda wa viongozi wa kanda ulikuwa ni wa muda na wa mpito hadi uchaguzi wa kanda utakapopita ambao ulipaswa kufanyika Juni 2014 na kwamba muda umeongezwa hivyo ameona aheshimu maagizo yaliyomweka madarakani.
 
Hata hivyo, Matare anasema kuwa anawatia moyo makamanda wote wa Chadema waliobaki kuendelea kupigania nchi ili iondokane na uovu unaotendeka sasa na kwamba Mungu atakuwa nao wale wote wanaotafuta haki kwa ajili ya wananchi walio wengi.

Rais Kikwete: Uchaguzi Serikali za Mitaa kusogezwa mbele


RAIS Jakaya Kikwete amesema uchaguzi wa serikali za mitaa ambao ulikuwa ufanyike mwezi Oktoba mwaka huu, huenda ukasogezwa mbele kutokana na kutokamilika kwa mchakato wa rasimu ya mabadiliko ya Katiba.
 
Kauli hiyo ameitoa kwenye mkutano wa majumuisho ya ziara yake ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Tanga.
 
Alisema kulingana na hali ilivyo hivi sasa ambapo Bunge la Katiba halijakamilisha kazi zake, ni dhahiri kwamba uwezekano wa kufanyika kwa uchaguzi huo kwa kutumia Katiba mpya haupo.
 
“Kwa mfano, wabunge endapo wataamua wapitishe kwamba katiba itambue serikali 3 ni lazima kwanza itungwe katiba ya Tanganyika ambayo itaainisha taratibu zitakazotoa mwongozo wa uchaguzi…hata kama itabaki kama ilivyo …. bado muda wa kuandaa huo utaratibu wa uchaguzi wa serikali za mitaa hautatosha kwa sasa”, alisema.
 
Aidha aliongeza, “Nimeona niliseme hili japo kwa ufupi kwamba uchaguzi huu huenda utalazimika kusogezwa mbele kutokana na kutokamilika kwa mchakato wa Rasimu ya mabadiliko ya Katiba“, alisema.
 
Katika hatua nyingine, Rais amewataka Maofisa Kilimo kwenye halmashauri kujiendeleza kitaaluma na kuwa mabingwa waliojikita katika taaluma ya mazao yanayostawi kwenye maeneo yao badala ya kuyashughulikia kwa ujumla mazao yote yanayolimwa na wananchi.
 
Alisema utekelezaji wa agizo hilo utaongeza mavuno kwa zao husika, utapanua wigo wa uzalishaji pamoja na utaalamu katika kushughulikia zao, aina ya zao na kuleta tija katika sekta ya kilimo.
 
Alisema hatua ya maofisa kilimo kuendelea kujishughulisha kwa ujumla na mazao yote yanayostawi bila kuwa na lengo la kusimamia mazao maalumu, kunaifanya sekta hiyo kudumaa na hivyo kushindwa kuwakwamua kiuchumi wananchi.
 
“Nimegundua kwamba watu wetu wengi hawana utaalamu uliobobea…hata maofisa kilimo wetu hawana taaluma maalumu zilizojikita kwenye aina ya mazao mengine zaidi ya mpunga na mahindi, hatua ambayo inawasababisha washindwe kusimamia vizuri uzalishaji wa mazao mengine ambayo yangeweza kuwakwamua kiuchumi wakulima kwenye halmashauri husika,” alisema.
 
Aliongeza, “Kwa hiyo ni jukumu lenu viongozi wa halmashauri kuwachukua maofisa kilimo wenu na kuwapeleka SUA kwa ajili ya ku-specialize (kujikita) kulingana na vipaumbele vyenu vya mazao kwa sababu sio wote wanao ubingwa katika kila zao…tukifanikiwa kwenye hilo tutapata mafanikio zaidi”, alisema.
 
Aidha aliwataka viongozi kwenye mkoa wa Tanga kuhakikisha shughuli za kilimo zinajikita kwenye uzalishaji endelevu wa mazao ya matunda na mboga, kwa kuwa mkoa huo uko katika fursa nzuri kiuzalishaji zaidi ya mazao ya nafaka.

Dayna Nyange asimulia jinsi anavyoshambuliwa na Mashabiki kwa Lugha Chafu baada ya kuamua Kujichubua


Mwimbaji wa kike Dayna Nyange amezungumzia jinsi alivyokutana na changamoto nyingi baada ya kuamua kubadili rangi ya  ngozi yake na kuwa nyeupe.
 
Akiongea katika The Jump Off ya 100.5 Times Fm, Dayna ameeleza kuwa amekuwa akikosolewa na watu wengi huku wengine wakitumia lugha mbaya dhidi yake lakini yeye ameipokea vizuri kwa kuwa anaamini ni watu wanaompenda.
 
“Ni sawa kwa sababu mimi naamini ni watu wangu wa karibu na ni watu ambao wananipenda ndio maana wanakuwa wanasema japo wengine wanatumia kauli mbaya. Lakini pia ni sawa kwa sababu mimi najua hao ni binadamu na kila binadamu anajua jinsi ya kupresent kwa mtu vile ambavyo anajisikia kwa hiyo ni mimi kutumia tu akili nakipokeaje.” Amesema Dayna Nyange.
 
Ameeleza kuwa yeye anaamini hakuna kitu ambacho aliwahi kukifanya kabla kikawa gumzo au tatizo kwa watu na ndio maana watu wanaamua kulichukulia hili kama tatizo kubwa.
 
Mwimbaji huyo alitangaza uamuzi aliouchukua kufuatia changamoto hizo alizokutana nazo ingawa anaamini kila mtu anauhuru wa kufanya maamuzi kama alivyoamua yeye.
 
“Kwa hiyo mimi naweza kusema ni sawa, inawezekana kweli nimekosa. Lakini mimi kama binadamu pia nina maamuzi yangu na nina sababu nyingi tu za kufanya kile ninachokifanya. Japo nimesikia maneno mengi sana mpaka Lol..’nimeacha.!
 
“Siwezi kusema kuwa nimeacha kabisa lakini nimetoka kule nilikokuwa, sasa hivi narudi kuwa Dayna yule ambaye mnataka awe. Japo pia binadamu pia mnakitu kimoja, sifieni kile kilicho bora kabla hakijakuwa sio.” Ameaongeza.

Rose Ndauka Amkimbia Mumewe


Staa wa filamu za Kibongo, Rose Ndauka hivi karibuni aliamua kumkimbia mumewe Malick Bandawe, kisa mfungo wa Ramadhani ambapo sasa anaishi Kigogo na mama yake mzazi. 

Akipiga stori na mwanahabari wetu, Rose alisema amelazimika kwenda nyumbani kwao ili kumpisha mumewe atimize nguzo hiyo ya Uislam bila kipingamizi kutokana na kutokufunga ndoa.
 
“Mimi sifungi hivyo nimeona pia ni jambo la busara kumpa nafasi mwenzangu kwa ajili ya kufanya ibada hiyo, mwezi ukiisha nitarudi na maisha yetu yataendelea kama kawaida,” alisema Rose ambaye awali alikuwa akiishi na mumewe huyo Tandale jijini Dar.

Mwanamke Aliyemng'ata Hausigeli na kumchoma Pasi Aachiwa


Mtuhumiwa wa kesi ya kujeruhi kwa kumng'ata sehemu mbalimbali za mwili  mfanyakazi wa ndani, inayomkabili Amina Maige (42) amepatiwa dhamana jana baada  ya mahakama kuthibitisha kuwa hasira kutoka kwa wananchi zimepungua.
 
Hakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni, Yohana Yongolo alisema ameridhishwa na ufafanuzi uliotolewa na Mwendesha mashitaka wa Serikali pamoja na Wakili wa mshitakiwa kuwa haki ya dhamana itolewe kwa kufuata masharti na kwamba hakuna uhalifu wowote utakaofanyika dhidi ya mshitakiwa huyo.
 
Hakimu  Yongolo alitoa masharti ya dhamana ambayo yalimtaka Maige kutoondoka nje ya Dar es salaam bila ya ruhusa ya mahakama hiyo.
 
Pia alitoa masharti ya kuwa na wadhamini wawili wa kuaminiwa kutoka taasisi inayotambulika hapa nchini ambapo mdhamini huyo anaweza kuwa mwajiriwa, mfanya biashara na mkulima.
 
Alisema wadhamini hao watatakiwa kusaini hati ya makubaliano kwa kila mmoja kulipa Sh milioni tatu.
 
Aliongeza kuwa kesi hiyo itasikilizwa Julai 22 mwaka huu.
 
Maige alidaiwa Januari mwaka jana hadi Juni mwaka huu, alimng'ata na kumchoma na  pasi  sehemu mbalimbali za mwili wa  mfanyakazi waje wa ndani Yusta Kashinde (20) na kumsababishia maumivu mwilini.

Mbio za Urais 2015: Fredrick Sumaye Asema yeye ndo Tumaini pekee la Watanzania


WAZIRI Mkuu Mstaafu, Fredrick Sumaye, amesema yeye ni tumaini la Watanzania na mpambanaji wa vita dhidi ya maovu.
 
Kutokana na hali hiyo, amesema ni jemadari hodari aliyeungana na askari wapiganaji hodari wa vita ambao wataleta ushindi usio na shaka.
 
Kauli hiyo aliitoa jijini Mwanza jana, katika hotuba yake ya uzinduzi wa taasisi ya Vijana ya Tanzania Youth (TYDC), ambako alipinga hatua ya baadhi ya wanasiasa kununua wapiga kura kwenye uchaguzi na kufanikisha kitendo hicho ni sawa na uroho wa  madaraka. 
 
Alisema hali hiyo ni hatari, kwani wanasiasa wa aina hiyo wanapaswa kuangaliwa kwa umakini wa hali ya juu, wanaweza kulisambaratisha Taifa.
 
Sumaye ni mmoja wa makada sita wa CCM waliopewa onyo kutokana na kile kilichoelezwa kuanza kampeni za kuwania urais kabla ya wakati.
 
Akizungumza na MTANZANIA baada ya uzinduzi wa taasisi hiyo, Sumaye alisema yupo tayari kugombea urais iwapo ataombwa kufanya hivyo.
 
Akijibu maswali kwa waandishi wa habari, alisema dhamira yake katika kujitosa kuwania urais ipo, lakini pale atakapoombwa kugombea.
 
“Nikiombwa kugombea urais nitagombea, hilo wala halina tatizo…na mjue kutangaza nia siyo kosa kwa mujibu wa kanuni za CCM, ila kosa ni kufanya kampeni kabla ya muda, wakati rais anapomaliza muda wake wagombea wengi hujitokeza kuwania nafasi hiyo, sasa hata mimi nikiombwa nitagombea,” alisema Sumaye.
 
Sumaye, anayetajwa kuwa miongoni mwa wanasiasa ndani ya CCM wanaotaka kuwania urais mwaka 2015, akizungumza katika uzinduzi huo wa TYDC, alisema kuna watu wamekuwa wakitumia nguvu ya fedha kusaka madaraka na kuwafananisha na watu wafupi wanalazimisha kupanda juu ya stuli ili waonekane mbele ya jamii kwa kutumia nguvu kubwa ya fedha.
 
Alisema watu hao ni hatari iwapo wakichaguliwa na kushuka juu ya stuli kwa vile hawataonekana tena kuwasaidia wananchi na kubainisha wamekuwa wakiwatumia vijana vibaya ili kukidhi malengo yao binafsi, yakiwemo ya kisiasa.
 
Katika kongamano hilo, Sumaye alitangaza kuwa mlezi wa vijana nchini na kuwaahidi maisha ya matumaini kwa miaka ijayo.
 
“Mimi nataka niwe mlezi wa vijana wa Tanzania nzima ili wawe na maisha ya matumaini. Ninyi vijana mtu akiwaleteeni hela chukueni kuleni halafu mnamchagua mwingine. Yaani hata Sumaye akileta msikatae hela, chukueni kuleni msimchague, maana mtu anayetumia nguvu ya fedha kusaka madaraka ya Serikali za Mitaa, udiwani, ubunge na hata urais huyo hafai na ni dhaifu,” alisema Sumaye, huku akieleza hakuja kwenye kongamano hilo kwa sababu za kisiasa.
 
Aliwaasa vijana wote, hususan waliopo masomoni wasidanganyike wala kutegemea kupata ajira za ofisini na kwamba wasiopata ajira wasikubali kutumiwa kisiasa, vijana watakaotumiwa watakuwa wamejiunga katika kundi la wala rushwa na wapokea rushwa, watakuwa wamejiunga kwenye kundi la mafisadi na la maangamizi kwa taifa.
 
Alisema kwamba vijana ni jeshi muhimu la taifa kwa maslahi ya taifa na wananchi wake na siyo jeshi la kuleta maafa katika jamii, hivyo atakuwa mlezi wa vijana kwa mambo yote na sifa anayoipenda ni mtu kuwa mzalendo wa kweli, kusimamia haki ya umma na siyo maslahi binafsi.
 
Alisema kwamba, hivi sasa Watanzania wanaelekea kwenye uchaguzi na fedha nyingi zinatembezwa kwa vijana ili watoa rushwa wachaguliwe katika nafasi wanazoomba na kudai siku hizi kumeibuka mtindo wa watoa fedha kuitwa wakarimu na wasiotoa kuhonga wao huitwa wachoyo.
 
“Mliponitaka niwe mlezi wenu nilikubali kwa sababu mimi ni mpambanaji wa vita dhidi ya matatizo na maovu hayo ambayo TYDC imeyaweka kama malengo yake makuu.
 
“Hivyo niliona nimepata wapiganaji wenzangu katika vita hii na kwa bahati nzuri wapiganaji wenyewe ni vijana ambao ni wengi, ni wenye nguvu na ndio wenye uchungu na nchi yao. 
"Mimi ninawaahidi kuwa mmempata jemadari hodari wa kuongoza vita hii na yeye jemadari amepata askari mashujaa wa kupigana vita hiyo,” alisema.
 
Alisema muunganiko huo wa wawili wa jemadari hodari na askari wapiganaji hodari wa vita utaleta ushindi usio na shaka.
 
“Kama unavyoambiwa wewe na wenzako wengine wasiokuwa na mahesabu nao huambiwa vivyo hivyo. Lakini la msingi ujue kuwa kama mtu anatumia njia hizo za mkato kutaka kuingia madarakani, huyo mtu hajiamini na wala hana uhakika na uwezo wake wa kumudu hayo madaraka anayoyatafuta, vinginevyo asingehangaika kuhonga watu,” alisema Sumaye.
 
Awali akimkaribisha Sumaye kuzungumza na halaiki ya vijana zaidi ya 300, Mwenyekiti wa TYDC, Lengai Thomas Ole Sabaya, alionekana wazi kumpigia ‘debe’ Sumaye katika harakati zake za kisiasa, kwa kusema wakati wa utawala wake na Mkapa fedha ya Tanzania ilikuwa na thamani kuliko ilivyo leo hii.
 
Sumaye alikuwa Waziri Mkuu kwa miaka 10 katika Serikali ya Rais Benjamin Mkapa.
Februari 18, mwaka huu, Chama Cha Mapinduzi (CCM), kupitia Kamati Ndogo ya Udhibiti na Nidhamu katika kikao chake ilipendekeza kuchukuliwa hatua za kinidhamu kwa makada wake ambao wameanza kampeni ya kuwania urais wa mwaka 2015.
 
Uamuzi huo wa kamati hiyo ya maadili ulibarikiwa na Kamati Kuu (CC) ya CCM, iliyokutana Februari 17, mwaka huu mjini Dodoma, chini ya Mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete.
 
Makada waliopewa adhabu ya mwaka mmoja kwa tuhuma za kuanza kampeni za kuwania urais kabla ya wakati ni January Makamba, Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa, Waziri Mkuu Mstaafu Frederick Sumaye, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe.
 
Wengine ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu) Steven Wassira pamoja na aliyewahi kuwa Waziri wa Nishati na Madini ambaye ni Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja.
 
Katika adhabu hiyo, makada hao walizuiwa kujihusisha na masuala ya kisiasa ndani ya chama hicho kwa miezi 12, huku mwenendo wao wa kisiasa ukifuatiliwa chini ya uangalizi mkali katika kipindi chote cha kutumikia adhabu hiyo.
 
Kabla ya adhabu hiyo, makada hao waliitwa na kuhojiwa na Kamati Ndogo ya Maadili ambayo iliwatia hatiani kwa kutumia Kitabu cha Kanuni ya Uongozi na Maadili ya CCM, toleo la Februari 2010, Ibara 6 (7)(i).

Credit: Mtanzania

VJ Penny Achumbiwa.....Sasa kuanza Maisha Mapya baada ya kutemana na Diamond


Mtangazaji maarufu nchini VJ Penny ambaye alikuwa mpenzi wa Diamond Platnumz amechumbiwa.  Kupitia Instagram Penny ameweka picha akiwa amevaa pete ya uchumba  na  kuandika  ujumbe  huu: “Road trip ….site her we come…cc @halimakimwana1.” 
Pia juzi  tulisikia   kuwa Penny amechumbiwa ingawa hatukupata habari kwa kina mpaka Penny mwenyewe alipoweka picha Instagram  akiwa  amevaa  pete  ya  Uchumba.

VJ Penny ambaye  inadaiwa alikuwa chaguo la kwanza la mama Diamond Platinumz ameweka picha hiyo siku moja baada ya Wema Sepetu kupost picha nyingi kwenye Instagram akiwa na mama Diamond kwenye sherehe ya siku yake ya kuzaliwa na kuzipa caption mbalimbali huku nyingine zikiwa na vijembe.
Tunampa hongera zote VJ Penny kwa  kuchumbiwa.