Askari mmoja wa kikosi cha usalama barabara ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja amenusurika kufa baada ya kupata ajali akiwa anaendesha pikipiki ya polisi ambayo ilikosa mwelekeo na kugongana uso kwa uso na gari dogo lenye namba za usajili T 681 CUX eneo la Bamaga Mikocheni jijini Dar es salaam ambapo gari hilo lilikuwa likiandeshwa na mwanamke mmoja huku mashuhuda wa ajali hiyo kila mmoja akiwa na mtazamo tofauti juu ya ajali hiyo.
Irene Uwoya amtaka Ndikumana Yanga, mwenyewe aogopa kulogwa.....Asema Uwoya bado ni Mke wake na wanapendana sana
BINTI aliyejaliwa uzuri wa sura anayeng’ara kwenye filamu za Kibongo, anamshawishi mumewe Hamad Ndikumana aje kucheza Yanga ya chini ya kocha, Marcio Maximo.
Ndikumana ambaye kwa sasa anaichezea Vital’o ya
Bujumbura, Burundi ameweka wazi kwamba binti huyo, Irene Uwoya ambaye ni
mkewe ni shabiki wa Jangwani na amekua akimshawishi kila mara kwamba
atue Jangwani ili awe naye karibu zaidi kwani hana mpango wa kuondoka
Dar es Salaam kwenye kazi zake za filamu.
Mchezaji huyo amekiri kushawishiwa mara nyingi
lakini alisema hawezi kujipeleka Yanga mpaka timu hiyo itakapomfuata,
kama hiyo haitoshi aliongeza kwamba anaogopa kuishi Dar es Salaam
kutokana na mambo ya ushirikina yaliyomtokea alipoanza maisha na mkewe
ambaye ameshangaa watu wanaozusha kwamba wameachana.
“Ananitaka nije kucheza Tanzania alikuwa
ananiambia nije Yanga, unajua anaipenda sana Yanga lakini nikamwambia
mimi ni mchezaji ninayejiamini siwezi kuja kuomba Yanga wanisajili acha
waje wao tuzungumze, yuko tayari kufanya hata ushawishi kwa wadau,”
anasisitiza Ndikumana ambaye awali alikuwa akiichezea APOP Kinyras
Peyias ya Cyprus.
Ndikumana alisema kilichomtoa Cyprus na kuja Burundi pamoja na uhusiano wake na Uwoya.
“Kweli nilikuwa Cyprus kama unavyosema lakini
kikubwa ambacho kilinirudisha Tanzania ni pale mke wangu alipokaribia
kujifungua, niliporudi tu baada ya muda nikaanza kuumwa sana na hivyo
kushindwa kurudi Cyprus,” anasimulia.
“Tatizo hilo naweza kusema ni mambo yetu ya
Kiswahili na ni huko Tanzania ndiyo kulikuwa chanzo, kuna vitu vilikuwa
vinanitokea mwilini kiasi kwamba nilikuwa najikuna sana mwili mzima,
hospitali nilikwenda na kupima vipimo vyote hakukuonekana kitu, kuna
wakati wakaniambia ni fangasi.
“Nikaona hapana bora nigeukie upande wa pili wa
tiba asilia, nako hali haikuwa rahisi nilizidi kuteseka ilifikia hatua
najikuna mpaka vidonda vinatoka miguuni nikaona sasa na vidonda hivi
nitarudije Cyprus bora nitibiwe kwanza kabla ya kuondoka.
“Ukweli ni kwamba nilizunguka sana kwa wataalamu
mbalimbali kiu yangu ilikuwa ni kuhakikisha nakuwa sawa, nakumbuka
mwanzoni kama ndani ya miezi miwili nilitumia hadi Sh6milioni kusaka
tiba lakini bado ikashindikana, nilikuwa nataka kuhakikisha napona
haraka ili niwahi kurudi kazini.
“Nilizunguka sana nakumbuka baada ya kuona
Tanzania ni vigumu nikaondoka na kuja hapa Rwanda nako nilitibiwa hali
haikuwa sawa, nikaenda DR Congo kidogo nikapata nafuu lakini baadaye
kuna mtalaamu mmoja akanisaidia tena kwa kiasi kidogo maradhi
yakapungua.
“Kuna mtu namjua kwamba alikuwa akifanya haya
yote, hili nililiamini baada ya kumrudia Mungu, ukiacha ya Mungu pia
hata hao wataalamu karibu wote nilipokuwa napita walikuwa wakimtaja
sioni kama walikuwa wanadanganya kwani ni watu tofauti wote wamemtaja
mtu mmoja, namuachia Mungu na nashukuru sasa nimeanza kurudi katika hali
yangu.
“Baada ya misukosuko yote hiyo Baba yangu
(Ndikumana Kitenge) kule nyumbani ana timu yake ndogo ya vijana, nikawa
natumia muda huo kumsaidia majukumu ya kuwafundisha vijana na hapohapo
na mimi nafanya mazoezi, nilipoona hali imeimarika nikaenda Vital’O
kuwaomba nifanye nao kazi wakakubali na nashukuru walinielewa na
kuniamini sasa nipo nao kwa muda.
“Sijasaini mkataba na Vital’O unajua kuna wakati nafanya
mazoezi kuna timu za Ulaya zilikuwa zinataka kunifuata nikaona niende
Vital’O ili nijiweke sawa endapo watakuja wanikute katika hali nzuri
lakini hao jamaa walivutiwa na mimi wakati nacheza kama beki na sasa
hapa natumika kama kiungo mkabaji sijajua kama wakija watanikubali.”
Alikutana wapi na Uwoya?
“Unajua Irene nilimpenda kupitia filamu
nilipomuona nikataka siku moja nikutane naye, nashukuru Mungu kuna siku
wakati nataka kwenda Kigoma katika harusi ya dada yangu nilipitia Dar es
Salaam nikakutana naye pale uwanja wa ndege.
“Sijabadili dini, ni kweli kwamba tulifunga ndoa
ya kanisani lakini sikubadili dini nilitajwa kwa jina la Hamad
Ndikumana, tulikubaliana na mke wangu tufunge ndoa mbili ya Kikristo na
Kiislamu ikatangulia ile hii nyingine tukasema tutaifunga baadaye lakini
muda ukawa mdogo ila tutaifunga hakuna shida.
Ni kweli wameachana na Uwoya?
“Kwanza nashangaa hao wanaodai nimeachana na mke
wangu wanajua nani amempa talaka mwenzake? Sijaachana na Uwoya, yule ni
mke wangu isipokuwa kwa sasa ni kama tumetengana na huko si kuachana
labda watu wanachanganya mambo.
“Kuna mambo tulishindwa kukubaliana, alikuwa
hataki kuja kuishi na mimi kule Cyprus, alikuwa anataka tuishi Tanzania
tu, sasa mimi kazi yangu ni soka siwezi kuacha kazi ili nirudi Tanzania
niishi na familia yangu bila ya kuwa na kazi hilo lilitufanya tutengane
kidogo.
“Achana na mtoto nipo na maelewano mazuri na Uwoya
hadi sasa tunawasiliana ngoja nikuthibitishie (Anainua simu na kumpigia
lakini haipokelewi) nadhani atakuwa katika kazi zake, yupo safarini
Afrika Kusini amekwenda kurekodi filamu na hata Krish ni mwanangu kila
ninapotaka kumuona namuona bila shida.
“Sasa ana miaka mitatu na tumeshamwanzisha shule,
anasoma (ananionyesha video fupi Krish aliyorekodiwa akihesabu namba kwa
Kiingereza) nadhani sasa utaniamini unajua watu hawajui mimi na Irene
ni wapenzi na tunaonana kila tunapopata nafasi.
“Hayo ni maneno ya watu tu, unajua Tanzania maneno
ni mengi sana, kweli kuna wakati yanasemwa mengi sana ninaposikia
nakutana na mwenzangu namuuliza anakataa lakini ukiacha kukataa kwake
hata mimi nimeshindwa kuthibitisha hayo madai kwa hiyo nayaacha maisha
yanaendelea.
“Kila kitu kina muda wake bado naamini siku moja
nitarudi kuwa karibu na familia yangu, kwa sasa acha kwanza kila mmoja
afanye yake ya kikazi, baadaye tutatulia na kuwa pamoja, watu waache
kutugombanisha,”anasisitiza.
Chanzo: Mwanaspoti
Chanzo: Mwanaspoti
Baba amuingilia bintiye kinyume cha maumbile
Vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia bado vinaendelea Zanzibar baada ya watu wawili kushikiliwa na polisi kwa tuhuma za kubaka.
Katika tukio lililotokea Agosti 4, mwaka huu Muhammed Khafidh Thabit
(50), anadaiwa kumbaka mtoto wake wa kumzaa mwenye umri wa miaka 14.
Mtuhumiwa huyo alimuingilia binti yake huyo kinyume na maumbile na kumsababishia madhara makubwa mwilini wake.
Akizungumzia kuhusu tukio hilo, Kamanda wa Polisi mkoa wa Mjini
Magharibi Unguja, Mkadam Khamis Mkadam, alisema tukio hilo limetokea
eneo la Misufini.
Alisema baada ya kuhojiwa mtoto huyo, alisema baba yake alikuwa
akimlazimisha kufanya mapenzi baada ya mama yake kutengana na baba huyo.
Alisema uchunguzi wa kidaktari umeonesha kuwa mtoto huyo ameingiliwa mbele na nyuma.
Katika tukio lingine la mkoa wa Kusini Unguja Polisi inamshikilia Ali
Hashim Ali (27) mkazi wa Mwera visiwani hapa kwa tuhuma za kumuingilia
mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka tisa.
Kamanda wa polisi mkoani humo, Juma Said Khamis alisema kijana huyo
alimrubuni mtoto huyo kwa kumuahidi kuwa atampatia mbuzi wa kufuga.
Alisema mtuhumiwa huyo alimchukua mtoto huyo na kumpeleka katika boma la nyumba na kumfanyia kitendo hicho cha kinyama.
Alisema mtuhumiwa ameshawahi kuwalawiti watoto wengine wawili wa kiume.
Watuhumiwa wote wapo chini ya ulinzi.
Akihutubia Baraza la Idi hivi karibuni, Dk Ali Muhammed Shein alikemea vitendo vya udhalilishaji na kutaka vipigwe vita.
Alisema takwimu za vitendo vya udhalilishaji zinaonesha kuendelea kuwepo
kwa vitendo hivyo licha ya jitihada zinazochukuliwa na serikali na
kushiriana na wanaharakati.
Credit: Nipashe
Kanisa lawataka wachungaji wajiuzulu CHADEMA
Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Kusini ambaye pia ni Mchungaji wa Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT), Joseph Matare amejiuzulu nafasi yake hiyo kutokana na kanisa lake kuwataka wachungaji wake ambao ni viongozi wa vyama vya siasa kuachana na nafasi zao za kisiasa.
Joseph Matare akizungumza na waandishi wa habari
mjini Songea amesema kuwa ameamua kujiuzulu nafasi yake ya uongozi wa
Chadema Kanda ya Kusini inayojumuisha mikoa ya Lindi, Mtwara na Ruvuma
baada ya kanisa lake katika mkutano wake wa kanda kuagiza wachungaji
wake ambao ni viongozi wa siasa kuachia nafasi zao na badala yake
wasimamie kazi ya Mungu katika makanisa yao.
“Kufuatia maagizo ya mkutano huo wa kanisa
uliofanyika Njombe nimeamua kutii... nimeamua kujiuzulu na katibu wangu
mkuu, Dk Willibrod Slaa nilimjulisha tangu tarehe 4 Juni mwaka huu,”
alisema Matare katika taarifa yake ya kujiuzulu.
Amefafanua kuwa muda wa viongozi wa kanda ulikuwa
ni wa muda na wa mpito hadi uchaguzi wa kanda utakapopita ambao ulipaswa
kufanyika Juni 2014 na kwamba muda umeongezwa hivyo ameona aheshimu
maagizo yaliyomweka madarakani.
Hata hivyo, Matare anasema kuwa anawatia moyo
makamanda wote wa Chadema waliobaki kuendelea kupigania nchi ili
iondokane na uovu unaotendeka sasa na kwamba Mungu atakuwa nao wale wote
wanaotafuta haki kwa ajili ya wananchi walio wengi.
Rais Kikwete: Uchaguzi Serikali za Mitaa kusogezwa mbele
RAIS Jakaya Kikwete amesema uchaguzi wa serikali za mitaa ambao ulikuwa ufanyike mwezi Oktoba mwaka huu, huenda ukasogezwa mbele kutokana na kutokamilika kwa mchakato wa rasimu ya mabadiliko ya Katiba.
Kauli hiyo ameitoa kwenye mkutano wa majumuisho ya ziara yake ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani Tanga.
Alisema
kulingana na hali ilivyo hivi sasa ambapo Bunge la Katiba
halijakamilisha kazi zake, ni dhahiri kwamba uwezekano wa kufanyika kwa
uchaguzi huo kwa kutumia Katiba mpya haupo.
“Kwa
mfano, wabunge endapo wataamua wapitishe kwamba katiba itambue serikali
3 ni lazima kwanza itungwe katiba ya Tanganyika ambayo itaainisha
taratibu zitakazotoa mwongozo wa uchaguzi…hata kama itabaki kama ilivyo
…. bado muda wa kuandaa huo utaratibu wa uchaguzi wa serikali za mitaa
hautatosha kwa sasa”, alisema.
Aidha aliongeza,
“Nimeona niliseme hili japo kwa ufupi kwamba uchaguzi huu huenda
utalazimika kusogezwa mbele kutokana na kutokamilika kwa mchakato wa
Rasimu ya mabadiliko ya Katiba“, alisema.
Katika
hatua nyingine, Rais amewataka Maofisa Kilimo kwenye halmashauri
kujiendeleza kitaaluma na kuwa mabingwa waliojikita katika taaluma ya
mazao yanayostawi kwenye maeneo yao badala ya kuyashughulikia kwa ujumla
mazao yote yanayolimwa na wananchi.
Alisema
utekelezaji wa agizo hilo utaongeza mavuno kwa zao husika, utapanua
wigo wa uzalishaji pamoja na utaalamu katika kushughulikia zao, aina ya
zao na kuleta tija katika sekta ya kilimo.
Alisema
hatua ya maofisa kilimo kuendelea kujishughulisha kwa ujumla na mazao
yote yanayostawi bila kuwa na lengo la kusimamia mazao maalumu,
kunaifanya sekta hiyo kudumaa na hivyo kushindwa kuwakwamua kiuchumi
wananchi.
“Nimegundua
kwamba watu wetu wengi hawana utaalamu uliobobea…hata maofisa kilimo
wetu hawana taaluma maalumu zilizojikita kwenye aina ya mazao mengine
zaidi ya mpunga na mahindi, hatua ambayo inawasababisha washindwe
kusimamia vizuri uzalishaji wa mazao mengine ambayo yangeweza kuwakwamua
kiuchumi wakulima kwenye halmashauri husika,” alisema.
Aliongeza, “Kwa
hiyo ni jukumu lenu viongozi wa halmashauri kuwachukua maofisa kilimo
wenu na kuwapeleka SUA kwa ajili ya ku-specialize (kujikita) kulingana
na vipaumbele vyenu vya mazao kwa sababu sio wote wanao ubingwa katika
kila zao…tukifanikiwa kwenye hilo tutapata mafanikio zaidi”, alisema.
Aidha
aliwataka viongozi kwenye mkoa wa Tanga kuhakikisha shughuli za kilimo
zinajikita kwenye uzalishaji endelevu wa mazao ya matunda na mboga, kwa
kuwa mkoa huo uko katika fursa nzuri kiuzalishaji zaidi ya mazao ya
nafaka.
Dayna Nyange asimulia jinsi anavyoshambuliwa na Mashabiki kwa Lugha Chafu baada ya kuamua Kujichubua
Mwimbaji wa kike Dayna Nyange amezungumzia jinsi alivyokutana na changamoto nyingi baada ya kuamua kubadili rangi ya ngozi yake na kuwa nyeupe.
Akiongea katika The Jump Off ya 100.5 Times Fm, Dayna ameeleza kuwa
amekuwa akikosolewa na watu wengi huku wengine wakitumia lugha mbaya dhidi
yake lakini yeye ameipokea vizuri kwa kuwa anaamini ni watu
wanaompenda.
“Ni sawa kwa sababu mimi naamini ni watu wangu wa karibu na ni watu
ambao wananipenda ndio maana wanakuwa wanasema japo wengine wanatumia
kauli mbaya. Lakini pia ni sawa kwa sababu mimi najua hao ni binadamu na
kila binadamu anajua jinsi ya kupresent kwa mtu vile ambavyo anajisikia
kwa hiyo ni mimi kutumia tu akili nakipokeaje.” Amesema Dayna Nyange.
Ameeleza kuwa yeye anaamini hakuna kitu ambacho aliwahi kukifanya
kabla kikawa gumzo au tatizo kwa watu na ndio maana watu wanaamua
kulichukulia hili kama tatizo kubwa.
Mwimbaji huyo alitangaza uamuzi aliouchukua kufuatia changamoto hizo
alizokutana nazo ingawa anaamini kila mtu anauhuru wa kufanya maamuzi
kama alivyoamua yeye.
“Kwa hiyo mimi naweza kusema ni sawa, inawezekana kweli nimekosa.
Lakini mimi kama binadamu pia nina maamuzi yangu na nina sababu nyingi
tu za kufanya kile ninachokifanya. Japo nimesikia maneno mengi sana
mpaka Lol..’nimeacha.!
“Siwezi kusema kuwa nimeacha kabisa lakini nimetoka kule nilikokuwa,
sasa hivi narudi kuwa Dayna yule ambaye mnataka awe. Japo pia binadamu
pia mnakitu kimoja, sifieni kile kilicho bora kabla hakijakuwa sio.”
Ameaongeza.
Rose Ndauka Amkimbia Mumewe
Staa wa filamu za Kibongo, Rose Ndauka hivi karibuni aliamua kumkimbia mumewe Malick Bandawe, kisa mfungo wa Ramadhani ambapo sasa anaishi Kigogo na mama yake mzazi.
Akipiga stori na mwanahabari wetu, Rose alisema amelazimika kwenda nyumbani
kwao ili kumpisha mumewe atimize nguzo hiyo ya Uislam bila kipingamizi
kutokana na kutokufunga ndoa.
“Mimi sifungi hivyo nimeona pia ni jambo la busara kumpa nafasi
mwenzangu kwa ajili ya kufanya ibada hiyo, mwezi ukiisha nitarudi na
maisha yetu yataendelea kama kawaida,” alisema Rose ambaye awali alikuwa
akiishi na mumewe huyo Tandale jijini Dar.
Mwanamke Aliyemng'ata Hausigeli na kumchoma Pasi Aachiwa
Mtuhumiwa wa kesi ya kujeruhi kwa kumng'ata sehemu mbalimbali za mwili mfanyakazi wa ndani, inayomkabili Amina Maige (42) amepatiwa dhamana jana baada ya mahakama kuthibitisha kuwa hasira kutoka kwa wananchi zimepungua.
Hakimu
wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni, Yohana Yongolo alisema
ameridhishwa na ufafanuzi uliotolewa na Mwendesha mashitaka wa Serikali
pamoja na Wakili wa mshitakiwa kuwa haki ya dhamana itolewe kwa kufuata
masharti na kwamba hakuna uhalifu wowote utakaofanyika dhidi ya
mshitakiwa huyo.
Hakimu
Yongolo alitoa masharti ya dhamana ambayo yalimtaka Maige kutoondoka
nje ya Dar es salaam bila ya ruhusa ya mahakama hiyo.
Pia
alitoa masharti ya kuwa na wadhamini wawili wa kuaminiwa kutoka taasisi
inayotambulika hapa nchini ambapo mdhamini huyo anaweza kuwa mwajiriwa,
mfanya biashara na mkulima.
Alisema wadhamini hao watatakiwa kusaini hati ya makubaliano kwa kila mmoja kulipa Sh milioni tatu.
Aliongeza kuwa kesi hiyo itasikilizwa Julai 22 mwaka huu.
Maige
alidaiwa Januari mwaka jana hadi Juni mwaka huu, alimng'ata na kumchoma
na pasi sehemu mbalimbali za mwili wa mfanyakazi waje wa ndani Yusta
Kashinde (20) na kumsababishia maumivu mwilini.
Mbio za Urais 2015: Fredrick Sumaye Asema yeye ndo Tumaini pekee la Watanzania
WAZIRI Mkuu Mstaafu, Fredrick Sumaye, amesema yeye ni tumaini la Watanzania na mpambanaji wa vita dhidi ya maovu.
Kutokana na hali hiyo, amesema ni jemadari hodari aliyeungana na
askari wapiganaji hodari wa vita ambao wataleta ushindi usio na shaka.
Kauli hiyo aliitoa jijini Mwanza jana, katika hotuba yake ya uzinduzi
wa taasisi ya Vijana ya Tanzania Youth (TYDC), ambako alipinga hatua ya
baadhi ya wanasiasa kununua wapiga kura kwenye uchaguzi na kufanikisha
kitendo hicho ni sawa na uroho wa madaraka.
Alisema hali hiyo ni hatari, kwani wanasiasa wa aina hiyo wanapaswa
kuangaliwa kwa umakini wa hali ya juu, wanaweza kulisambaratisha Taifa.
Sumaye ni mmoja wa makada sita wa CCM waliopewa onyo kutokana na kile
kilichoelezwa kuanza kampeni za kuwania urais kabla ya wakati.
Akizungumza na MTANZANIA baada ya uzinduzi wa taasisi hiyo, Sumaye
alisema yupo tayari kugombea urais iwapo ataombwa kufanya hivyo.
Akijibu maswali kwa waandishi wa habari, alisema dhamira yake katika
kujitosa kuwania urais ipo, lakini pale atakapoombwa kugombea.
“Nikiombwa kugombea urais nitagombea, hilo wala halina tatizo…na mjue
kutangaza nia siyo kosa kwa mujibu wa kanuni za CCM, ila kosa ni
kufanya kampeni kabla ya muda, wakati rais anapomaliza muda wake
wagombea wengi hujitokeza kuwania nafasi hiyo, sasa hata mimi nikiombwa
nitagombea,” alisema Sumaye.
Sumaye, anayetajwa kuwa miongoni mwa wanasiasa ndani ya CCM wanaotaka
kuwania urais mwaka 2015, akizungumza katika uzinduzi huo wa TYDC,
alisema kuna watu wamekuwa wakitumia nguvu ya fedha kusaka madaraka na
kuwafananisha na watu wafupi wanalazimisha kupanda juu ya stuli ili
waonekane mbele ya jamii kwa kutumia nguvu kubwa ya fedha.
Alisema watu hao ni hatari iwapo wakichaguliwa na kushuka juu ya
stuli kwa vile hawataonekana tena kuwasaidia wananchi na kubainisha
wamekuwa wakiwatumia vijana vibaya ili kukidhi malengo yao binafsi,
yakiwemo ya kisiasa.
Katika kongamano hilo, Sumaye alitangaza kuwa mlezi wa vijana nchini na kuwaahidi maisha ya matumaini kwa miaka ijayo.
“Mimi nataka niwe mlezi wa vijana wa Tanzania nzima ili wawe na
maisha ya matumaini. Ninyi vijana mtu akiwaleteeni hela chukueni kuleni
halafu mnamchagua mwingine. Yaani hata Sumaye akileta msikatae hela,
chukueni kuleni msimchague, maana mtu anayetumia nguvu ya fedha kusaka
madaraka ya Serikali za Mitaa, udiwani, ubunge na hata urais huyo hafai
na ni dhaifu,” alisema Sumaye, huku akieleza hakuja kwenye kongamano
hilo kwa sababu za kisiasa.
Aliwaasa vijana wote, hususan waliopo masomoni wasidanganyike wala
kutegemea kupata ajira za ofisini na kwamba wasiopata ajira wasikubali
kutumiwa kisiasa, vijana watakaotumiwa watakuwa wamejiunga katika kundi
la wala rushwa na wapokea rushwa, watakuwa wamejiunga kwenye kundi la
mafisadi na la maangamizi kwa taifa.
Alisema kwamba vijana ni jeshi muhimu la taifa kwa maslahi ya taifa
na wananchi wake na siyo jeshi la kuleta maafa katika jamii, hivyo
atakuwa mlezi wa vijana kwa mambo yote na sifa anayoipenda ni mtu kuwa
mzalendo wa kweli, kusimamia haki ya umma na siyo maslahi binafsi.
Alisema kwamba, hivi sasa Watanzania wanaelekea kwenye uchaguzi na
fedha nyingi zinatembezwa kwa vijana ili watoa rushwa wachaguliwe katika
nafasi wanazoomba na kudai siku hizi kumeibuka mtindo wa watoa fedha
kuitwa wakarimu na wasiotoa kuhonga wao huitwa wachoyo.
“Mliponitaka niwe mlezi wenu nilikubali kwa sababu mimi ni mpambanaji
wa vita dhidi ya matatizo na maovu hayo ambayo TYDC imeyaweka kama
malengo yake makuu.
“Hivyo niliona nimepata wapiganaji wenzangu katika vita hii na kwa
bahati nzuri wapiganaji wenyewe ni vijana ambao ni wengi, ni wenye nguvu
na ndio wenye uchungu na nchi yao.
"Mimi ninawaahidi kuwa mmempata
jemadari hodari wa kuongoza vita hii na yeye jemadari amepata askari
mashujaa wa kupigana vita hiyo,” alisema.
Alisema muunganiko huo wa wawili wa jemadari hodari na askari wapiganaji hodari wa vita utaleta ushindi usio na shaka.
“Kama unavyoambiwa wewe na wenzako wengine wasiokuwa na mahesabu nao
huambiwa vivyo hivyo. Lakini la msingi ujue kuwa kama mtu anatumia njia
hizo za mkato kutaka kuingia madarakani, huyo mtu hajiamini na wala hana
uhakika na uwezo wake wa kumudu hayo madaraka anayoyatafuta, vinginevyo
asingehangaika kuhonga watu,” alisema Sumaye.
Awali akimkaribisha Sumaye kuzungumza na halaiki ya vijana zaidi ya
300, Mwenyekiti wa TYDC, Lengai Thomas Ole Sabaya, alionekana wazi
kumpigia ‘debe’ Sumaye katika harakati zake za kisiasa, kwa kusema
wakati wa utawala wake na Mkapa fedha ya Tanzania ilikuwa na thamani
kuliko ilivyo leo hii.
Sumaye alikuwa Waziri Mkuu kwa miaka 10 katika Serikali ya Rais Benjamin Mkapa.
Februari 18, mwaka huu, Chama Cha Mapinduzi (CCM), kupitia Kamati
Ndogo ya Udhibiti na Nidhamu katika kikao chake ilipendekeza kuchukuliwa
hatua za kinidhamu kwa makada wake ambao wameanza kampeni ya kuwania
urais wa mwaka 2015.
Uamuzi huo wa kamati hiyo ya maadili ulibarikiwa na Kamati Kuu (CC)
ya CCM, iliyokutana Februari 17, mwaka huu mjini Dodoma, chini ya
Mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete.
Makada waliopewa adhabu ya mwaka mmoja kwa tuhuma za kuanza kampeni
za kuwania urais kabla ya wakati ni January Makamba, Waziri Mkuu wa
zamani Edward Lowassa, Waziri Mkuu Mstaafu Frederick Sumaye, Waziri wa
Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe.
Wengine ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu) Steven
Wassira pamoja na aliyewahi kuwa Waziri wa Nishati na Madini ambaye ni
Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja.
Katika adhabu hiyo, makada hao walizuiwa kujihusisha na masuala ya
kisiasa ndani ya chama hicho kwa miezi 12, huku mwenendo wao wa kisiasa
ukifuatiliwa chini ya uangalizi mkali katika kipindi chote cha kutumikia
adhabu hiyo.
Kabla ya adhabu hiyo, makada hao waliitwa na kuhojiwa na Kamati Ndogo
ya Maadili ambayo iliwatia hatiani kwa kutumia Kitabu cha Kanuni ya
Uongozi na Maadili ya CCM, toleo la Februari 2010, Ibara 6 (7)(i).
Credit: Mtanzania
VJ Penny Achumbiwa.....Sasa kuanza Maisha Mapya baada ya kutemana na Diamond
Mtangazaji maarufu nchini VJ Penny ambaye alikuwa mpenzi wa Diamond Platnumz amechumbiwa. Kupitia Instagram Penny ameweka picha akiwa amevaa pete ya uchumba na kuandika ujumbe huu: “Road trip ….site her we come…cc @halimakimwana1.”
Pia juzi tulisikia kuwa Penny amechumbiwa ingawa
hatukupata habari kwa kina mpaka Penny mwenyewe alipoweka picha Instagram
akiwa amevaa pete ya Uchumba.
VJ Penny ambaye inadaiwa alikuwa
chaguo la kwanza la mama Diamond Platinumz ameweka picha hiyo siku moja
baada ya Wema Sepetu kupost picha nyingi kwenye Instagram akiwa na mama
Diamond kwenye sherehe ya siku yake ya kuzaliwa na kuzipa caption
mbalimbali huku nyingine zikiwa na vijembe.
Tunampa hongera zote VJ Penny kwa kuchumbiwa.



















